Mshana Jr ( @Cage clay ) alimuuliza rafiki yake Kiranga kule nyumbani kama ana akili, Kiranga naye akataka kueleweshwa akili ni nini kabla ya kujibu kama ana akili ama hana akili, mjadala ukaishia hapo. Lakini swali kwamba watanzania tuna akili ama la ni swali linalotakiwa kumtafakarisha kila mtanzania kutokana na aina ya maisha tunayoishi.
Kama tuna akili je tunazitumia ipasavya na itakiwavyo. Hivi malezi ya kwenye familia zetu yanatupa nafasi ya kutumia mbongo zetu kwa kiwango cha kutunza ubinadamu wetu? Kuna tofauti gani kati yetu sisi na Roboti iliyoprogramiwa na kuendeshwa na mtengenezaji wake atakavyo?
Inategemeana na akili yako ikoje! Inawezekana unaona swali lako ni gumu na limepewa jibu rahisi, kumbe umepewa jibu gumu lisilolingana na uzito wa swali lako!
QUOTE=“Allen Kilewella, post: 1667403, member: 37285”]Kweli kwa neema maana walipofunga walitamani watufunge na sisi tusiwe na akili ya kufanya ukimbizi!!
[/QUOTE]
Hahahahaa ndio maana nikasema watz tuna akili tunatofautiana mauwezo tuu ya ung’amuzi