Una kipato cha kutosha, Mama na Baba yako walikuwa hawana kama wewe walizaa watoto zaidi ya 9.
Unasema watoto wengi hutaweza kuwalea ilihali una una uwezo wa kuwalea na kuwatimizia mahitaji yao yote, Mama na Baba yako ambao hawakiwa na huo uwezo waliweza kukulea wewe na ndugu zako wote zaidi ya 9 tena kwa kutegemea kilimo cha mvua za msimu.
Ninyi watoto mpo zaidi ya 9 ila mnashindwa kuwalea wazazi wenu 2 ilihali wao 2 waliweza kuwalea ninyi zaidi ya 9.
Hao watoto 2 uliowazaa unawalea malezi ya kuwadekeza hadi wanakuwa wakubwa hawajui hata kufua kitambaa cha kufutia kamasi, ukiugua hawawezi kukusaidia kisa malezi uliyowalea sio yale ya kujituma na kibaya zaidi kutokana na hizo tabia zao wakawa ni watoto wasio watiifu na kuwathamini wazazi wao, msaada unabaki kutegemea kwa majirani hadi wanachoka.
Ivi unajua anayegawa riziki ni muumba!!, kila mmoja anayezaliwa anakuwa na riziki yake ndio maana wazazi wenu waliweza kuwalea ninyi zaidi ya 9.
Kuoa/kuolewa ni sheria … kuzalisha/kuzaa ni majaliwa.
Wazazi wetu walikuwa wanagonga misosi ya maana. Siku hizi watu wanakula chipsi yai wanashushia na serengeti lite. Matokeo yake wanawake wana vitambi na wanaume wana wowowo… shahawa kama sabuni imekutana na maji