Wadau wa JF mnalionaje wazo la Jamiii Forums kujiunga na Kenyatalk permanently?

Pale kwenye Jamiiforums wabadili pawe Swahili Forums , ila majukwaa wayaache hivyo hivyo.
Naamini watu wengi bado tutaendelea kuwa humu hata JF ikiwa hewani.

Kwanini wasifungue kutokea nchi za nje kama USA, Europe? Why not register there. Mbona ansikia database ya JF iko Ufaransa, sasa kigumu ni nini kufungua Ufaransa?

sure! me nasemea wanaweza kuizuia sis tulio bongo tusiipate bt nchi zingne waipate

Ugenini kuna uhuru kuliko nyumbani

Mbona kama ni hivyo ni simple tu…watu watatumia VPN

Absolutely mkuu

Tangu JF infungwe darasa la Ras Simba lime over flow. Mimi nimekuwa class monitor.

Naona @Babu Asprin bado training haijamkaa vizuri kichwani maana anasua sua hapa sana

Wasio concentrate darasani utawajua tu

Absolutely true

Huyu Jiwe anadhani ana akili zaidi ya teknolojia

Sasa ameona ameifunga JF hapo nyumbani, wanaJF wanajiachia kwa nafasi kutoka nchi jirani!

Huyu Ngosha na wabunge wake wa CCM “weupe” kabisa upstairs…

Hii dunia ya Leo siyo ya kutumia mabavu bila kutumia akili, utaumbuka tuuu

Sasa Magufuli aibu imemkuta

Uzito wa miwani ya Babu napo unampa shida sana

Real talk,dunia ya leo bila kutumia akili ni sawa na bure

Mi nadhani hapa ugenini nini kuzuri tuu.hifadhi hii kama nini ya kudumu mbona poa tuu

Nipo nimetulia tele… tatizo vyuma vimekaza…

Yaani huyu Jiwe anadhani ametukomesha, kumbe ndiyo amejikomoa, kwa kuwa huku ukimbizini ndiyo tunajiachia kwa nafasi kubwa bila bughudha ya kutishwa tishwa

Bibi @Sky Eclat tunamsaidiaje huyu Babu…

Jibu ni gumu kwani mwenyewe amekiri hapa kuwa ana makoloni mengi. Lakini home kwetu hakuna vyuma.

Ugenini hasa kwa jirani sio permanent solution,kuna wakati serikali za majirani wanatengeneza MOU.
Kama Moi na Nyerere walivyobadirishana wale waliokuwa wakimbizi wa kisiasa kutoka nchi zetu yaani Kenya na Tanzania.Wale wakenya waliporudishwa walinyongwa.

Yaonekana tuna short memory.

Kwa sasa, ninachojua ni kwamba nipo kambi ya wakimbizi nikitafuta hifadhi, basi! Suala la kuwa permanent au temporally litajulikana hapo baadaye kulingana na hali halisi itakavyokuwa…

Lakini tambua kuwa mambo yote haya yanategemea nchi husika ina sheria gani…

Lazima tutambie kuwa Kenya haina sheria za “kijinga” kama za kwetu, kwa hiyo hata hiko unachokiita MoU haiwezi kufanya kazi kwa kuwa hata huyo Kenyatta keshamuona huyo mwenzake Magufuli kuwa “hamnazo” kwa upande wa upstairs