Kuna maiti ilipatikana chumbani ikining’inia darini, mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani na chumbani hapakuwa na kitanda, meza wala kiti. Chumba kilikuwa na ukubwa wa futi 14 mraba.
Sehemu ambapo marehemu alifunga kamba ni katikati ya dari, ambapo urefu kutoka pembe zote kutokea sehemu alipokuwa akining’inia marehemu ulikuwa sawa, pembeni palikuwa na paka amelala, na kando ya mlango palikuwa na maji sakafuni.
Je, ungelikuwa wewe ndiye mtaalamu wa uchunguzi (mpelelezi), hapa ungelitatuaje kisa hiki?
sina uhakika kama marehemu alijiua mwenyewe.kuna maswali yanakosa majibu.je alipanda juu ya dari?,alitokeaje kwa chini?dari ilikuwa na kijimlango?,kama majibu ni hapana.je alisimamia kitu gani mpaka akaikuta dari.hicho kitu alichosimamia kiko wapi ?