Siku zote najua jambo moja; Ukiingia mkataba na shetani tegemea 110% kuwa kutimiza wajibu kama ulivyoainishwa kwenye mkataba wenu hakukupi guarantee kuwa shetani nae ataheshimu mkataba wenu huo.
Hapana, huyu Mwigulu alipendwa sana na jiwe kwa ukatili wake na jinsi alivyokuwa aki dili kwa mkono na roho ya chuma kwa wapinzani. Kwake uhai au maumivu ya mpinzani kwake sio hoja kabisa.
Akapendwa na kujua yeye ndio yeye, kaja kuponzwa na msimamo wake Wa kuunga mkono waraka Wa KKKT na kusema wana haki ya kuandika walicho fikiri.
Hapo ikawa jiwe limetibuliwa nyongo hakuna mfano! Ni out tuu!
Sasa aje aombe radhi matukio aliyo kuwa anawafanyia wenzake. Na liwe somo jingine kwa washabiki Wa jiwe kuwa siku ukijitambua kidogo na ukawaza tofauti naye lazima akutose!
Nae ataanza kutweet kama Nape, ila ilishatabiriwa kitambo kwamba yeye na January ni suala la muda tu alikuwa anawatafuta ila walikuwa wanatembea kwa tahadhari sana, kaona isiwe tabu akamilishe adhma yake ya kuwatumbua, ila wote wamewatendea wanachi mambo mengi mabaya
Dakika ya 80 Mwigulu Lameck Nchemba anakwenda katika benchi… …Huku namuona HKigwangala akichungulingulia nje ya uwanja kama kuna mtu anapasha pasha achukue nafasi yake…!!!
Mtu kama Mwigulu akikutana na dhahama tena za kimamlaka roho yangu inafurahi ile mbaya. Katika watu waliondesha udhalimu nchi hii kupitia madaraka yeye ni mmoja wapo. Jamaa ana roho mbaya na mlevi wa madaraka. Hawa ndio siku utawala wa kulindana ukiondoka wanapaswa kuishia jela.
Mungu mkubwa, amesikia kilio cha watanzania hata kama aliyetengua nae the difference is the same. Damu ya watu kubomolewa hovyo nyumba zao na wengine kupoteza maisha, mauaji ya kibiti, masandarusi ya miili ya watu kuokotwa fukweni, watu kupotea, Lisu kupigwa lisasi mchana kweupe na mengineyo mengi dhamira ilipaswa kumuuma akajiuzuru mwenyewe. Au hata kuonyesha tu anaumi ila hanamamlaka kama alivyowahi sema bungeni ningekuwa na uwezo binge…leo. Hizi ndizo sifa za kijana msomi mwenye ndoto ya kuwa rais wa JMT.
You may be quite right. Kwa hakika yule Msajili wa Vyama vya Hiari hakujituma tu mwenyewe kuanza kuwapa ‘summons’ KKKT, TEC ofisini kwake na kuanza kuwauliza maswali ambayo hawapata kuulizwa tangu wazaliwe na kuwapa maagizo ya kufa mtu. Bila shaka alipokea maagizo ya kufanya hivyo, as sadistically as possible. Maadam maagizo hayakutoka wizarani basi ni ‘wasiojulikana’. Silly question: je, kwa mtaji huu ‘wasiojulikana’ hawajulikani kweli?