Nimekuwa nikisikia kuhusu uwepo wa uwezekano wa kusimamisha/kufunga ujauzito ili usikue kw kipindi ambacho mtu (mjamzito) atapenda, yaani mtu anaweza usubirisha ujauzito wake kwa kipindi hata cha miaka mitatu na baadae akaamua kuzaa.
Je kuna ukweli katika hili?
Naamini ugumu unaopitia kuielewa ndio uninaopitia pia. Ila kama ni suala la ujauzito, iko hivi.
Yaani mtu anapata ujauzito ukifikisha miezi kadhaa, yaweza kuwa miwili, mitatu au hata mmoja, anaenda kufanyiwa utaratibu wa kusimamisha ukuaji wa ujauzito, kwa kipindi atakachotaka mwenyewe (kama unavyo pause movie) kisha baadae akitaka anafanyiwa tena utaratibu na ujauzito unaendelea kukua (Anauresume).
Hii niliwahi isikia kwa mara ya kwanza mwaka jana nikaipuuzia lakini pia jana, nikiwa napiga stori na mdada mwingine tena akanambia hii kitu, kwa hiyo nikaona isiwe taabu nije kupata ufafanuzi toka kwa wanakijiji wenzangu