Hivi Rais Magufuli anapata kiburi chake kutokana na magari ya Polisi ya washawasha?

Nianze kwa kunukuu vifungu vya Katiba ya Jamhuri ya Muunhano wa Tanzania ya mwaka 1977, iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2005, ibara ya 3(1) ambayo inasema “Jamhuri ya Miungano wa Tanzania ni nchi ya kidemokrasia yenye kufuata mfumo wa vyama vingi” mwisho wa kunukuu

Duniani kote kwenye nchi inayofuata mfumo wa vyama vingi, tafsiri yake ni kuwa vyama vya upinzani, wajibu wake mkubwa ni kuikosoa serikali iliyoko madarakani ili ijirekebishe na kuwatendea haki wananchi
wake

Hebu ninukuu Ibara ya 18(1) ya Katiba hiyo hiyo ambayo inasema " Kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake na kutafuta, kupokea na kutoa habari zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi na pia Uhuru na mawasiliano hayo hayapaswi kuingiliwa na chombo kingine chochote" mwisho wa kunukuu

Nimejaribu kuvinukuu vifungu hivyo viwili ili tuone huyu Rais wetu anavyoisigina waziwazi Katiba ya nchi ambayo kabla ya kuingia madarakani aliapa kuwa ataitii Katiba hiyo

Kuhusu mfumo wa vyama vingi ni wazi kuwa wanachofanya viongozi wa upinzani kwa kuikosoa serikali iliyoko madarakani, ndiyo wajibu wao namba moja kwa wapiga kura wao

Tujiulize inakuwaje kiongozi wa upinzani anatekeleza wajibu wake kwa mujibu wa Katiba ya nchi, Jeshi la Polisi linamkamata kiongozi huyo na kumfungulia mashitaka ya uchochezi??

Tunajua kuwa Rais wetu Magufuli hataki kabisa kukosolewa, lakini Jeshi la Polisi linapaswa lifanye kazi yake kwa weledi wa kutojiegemeza na Chama chochote cha siasa na sivyo wanavyotekeleza wajibu wao kwa hivi sasa ambapo huwezi kuwatofautisha na UVCCM!

Tuje kwenye ile ibara ya 18(1) ya Katiba ambayo inatoa Uhuru kwa kila mwananchi kutoa maoni yake. Hivi tungeweza kweli sisi wananchi wa Tanzania kuwa wakimbizi nchini Kenya kwa ajili tu watawala wetu wameamua kuisigina Katiba ya nchi??

Nimekuwa nikijiuliza maswali mengi, hivi inakuwaje kwa Rais wa nchi kuamua kuisigina Katiba ya nchi waziwazi, ambayo kabla hatujamkabidhi madaraka hayo aliapa kuwa ataitii na kuilinda Katiba hiyo??

Nimekuwa pia nikijiuliza hivi huyu Rais Magufuli anapata wapi kiburi cha kuisigina Katiba ya nchi waziwazi??

Jibu ninalolipata ni kwa kujiona kwake kuwa ndiyo Commander in Chief wa majeshi yote nchini, kwa hiyo wapinzani hata mkiamua kuprotest kuhusu utawala wake, yeye ataviagiza vikosi vyake vya Polisi vije na magari ya washawasha ili viweze kuzima maandamano hayo!

Lakini kitu wanachosahau hayo majeshi ya Polisi ni kuwa hayo magari ya washawasha yananunuliwa na pesa za mlipa kodi wa nchi hii na mishahara ya hao Polisi inatokana na “kujisachi” mifukoni kwa tax payers

Kitu kimoja kilicho cha wazi ni kuwa kama kweli Bunge la nchi hii lingekuwa linafanya kazi yao wanayopaswa kuifanya ya kuisimamia serikali, basi lingekuwa limeshapiga kura ya kukosa imani kwa Rais wa nchi hii siku nyingi sana na Rais huyu angekuwa ameshatuachia huo Urais wetu

Ee Mwenyezi Mungu tujalie waja wako watanzania, na utuondolee huyu Magufuli ambaye ni dhahiri ame-abuse power yake

Vile CDF na IGP wanavyomnyenyekea anajiona yupo juu sheria, hajui wale wanamnyenyekea kwa sababu ya kiapo cha utiifu kwenye Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Yeye anajua wanamnyenyekea sababu ya mikwara yake…

We waache IGP na wenzake wanadhani nao wana kinga ya rais uzuri ni kwamba jinai haiexpire hata 2050 lazima wavune walichopanda labda wafe waishe wote

Huyo IGP ni lazima aburuzwe The Hague, kwa kuwa yapo mauaji ambayo yamefanywa na Polisi wake, lakini yeye anajaribu kiyafukia fukia…

Mfano dhahiri ni wa yule mwanafunzi wa NIT Akwlilina, ambapo DPP amefunga faili lake kwa madai kuwa eti wameshindwa kumbaini Muuaji!

Hao Polisi waliohusika na mauaji hayo watambue kuwa damu waliyoimwaga isiyo na hatia ya yule binti Akwilina itaendelea kuwalilia katika maisha yao yote hapa duniani

Dahh…

Tatizo ni sheria na kuogopana wao Kwa wao Polisi. Hawa Polisi wanajua kuna mambo wanavunja sheria na hata watu wa sisiem lakini wanafunga MACHO. Wanachokijua “Fuata sheria bila shuriti”. Ukiuliza ni sheria ipi imevunjwa kutokana na katiba ya nchi, wanakujibu " Maagizo kutoka juu". Sasa Tanzania tunaongozwa na Katiba ya nchi au na Maagizo kutoka juu?

Hapa ni lazima Polisi lijirudi ikiwezekana liwaombe wananchi radhi Kwa kukiuka katiba ya nchi na kufuata Maagizo ya CCM.

Kitu ambacho wao Polisi wanapaswa wakijue ni kuwa wao hawana kinga ya kutoshitakiwa…

Ambaye mwenye kinga hiyo pekee ni Rais wa nchi, kwa hiyo wao wanapaswa wafanye kazi yao kwa weledi na siyo kwa kufuata maagizo toka juu…

Nawakumbusha tu Kinga ya kutoguswa na vyombo vya dola anayo Rais tu, Kuna maisha baada ya utawala wake

Hivi kama kweli huyu Magufuli anawafanyia mema watanzania, huwa najiuliza ni kitu gani kinachomlazimisha awadhibiti viongozi wa upinzani kwa kiasi kikubwa hicho??

Nimekuwa pia najiuliza hivi hofu yake ni nini hadi kusababisha kuvidhibiti vyombo vya habari na hadi sasa kutufungia mtandao wetu pendwa wa JF??

Kwa kuwa kama kweli serikali yake ingekuwa inawafanyia mema watanzania, isingekuwa na hofu na “wasema ovyo”

Kwa kuwa imenenwa kuwa kizuri chajiuza na kibaya chajitembeza…

Kwa hiyo ni wajibu wetu sisi watanzania kuamua ni CCM inayojiuza au inayojitembeza. …

Lakini hiki kitu kinachofanyika kwa mtu anayeikosoa serikali “kumpyupyu” kinaonyesha kuwa anachofanya Magufuli ni guilty consciousness…

Na kutokana na ukweli huo yeye Jiwe ataingia katika historia ya kuwa ndiye “aliyekwapua” kupita Rais wowote tokea tupate Uhuru wetu

Hebu tujiulize ziko wapi shilingi 1.5 trillion zetu ambazo CAG alizibainisha kuwa “zimeyeyuka” kutoka kwenye hazina yetu??

Mkuu kama taifa tunatatizo kubwa lakutokutambua wajibu wetu kuanzia sisi raia mpaka viongozi wetu yaani wanasahau kama cheo ni dhamana tuu. Ujue kuna KPI za kila nafasi kitu amabacho nahisi hawa viongozi saidizi wa Rais huenda hawajui au wanapuuza, wao badala ya kuzingatia weledi wana leta mahaba binafsi kwenye ofisi za uma, hii inatuangusha sana mwishoe kuna kua hakuna uweledi hivyo kila kitu kinakwenda kwa beat lake. Leo JIWE anakimbia kwa kasi ya 4G lakini kuelekea nyuma kibaya kuna wanao piga miluzi kumpamba mkulu hii huenda inamchanganya anajua yupo kwenye LIYT TRAKI sisi wengine wakimbizi nikusubiri tuone mwisho ataleta swaga gani maana kama ni majipu katumbua hadi vidole vimeotaa sugu LAKINI TUMPE MUDA LABDA YULE MALAIKA ALIYE SHUKIA MITANDAO HUENDA ATAMSHUKIA NA YEYE PIA.

Hahaaaaaa…

Nimependa bandiko lako hususani pale uliposema kuwa LABDA MALAIKA KUTOKA MBINGUNI ALIYESHUKA NA KUIZIMA JF ATSHUKA NA KUMZIMA YEYE MWENYEWE!

Mkulima huvuna apandacho mkuu, Saizi anapalilia iko siku atavuna

Mkuu nijikite kwenye post yako namba moja. Ni kweli Magufuli hataki kukosolewa hilo kila mtu analifahamu; na hata yeye analifahamu fika na analitanalitenda kwa vitendo. Tatizo kubwa inaweza kuwa sio yeye kwani huo ni udhaifu wake, lakini vyama vya siasa hasa vya upinzani havijatekekeza wajibu wao. Vyama vya upinzani vilipaswa kwenda mahakamani kuhoji haki yao ya kikatiba lakini hilo hawajafanya. Ni kweli mahakama haiko huru hilo liko wazi, lakini walipaswa kwenda mahakamani kisha mahakama itoe tafsiri. Iwapo Magufuli asingetii amri ya mahakama hapo ingesaidia kuuambia umma uvunjwaji huo wa sheria.

Hakuna uwezekano wa kutegemea bunge limkanye Magufuli kwani nusu ya wabunge ambao ni wa ccm, wameingia madarakani kwa kupitia mfumo mbovu wa sheria za uchaguzi, na kitendo chochote cha kumrekebisha rais ambaye ni mwenyekiti wa chama chao ni hatari kwa chama na nafasi zao. Hivyo kitendo cha Magufuli kutumia nafasi yake kama rais kufanya apendavyo ndio salama ya yeye na chama chake kuendelea kupata ulaji kwa kuwa madarakani.

Kuhusu vyombo vya dola kutii amri toka juu na sio sheria. Hilo halitokaa liishe mpaka pale katiba itakapompunguzia rais madaraka ikiwapo kushitakiwa akiwa au ametoka madarakani. Mfumo uliopo wa kutoshitakiwa kwa rais akiwa madarakani au akiwa ametoka ndio chimbuko la udhaifu wa taasisi zote za nchi hii. Kitendo hiki ndio kimekuwa mbadala wa sheria za nchi na amri kutoka juu ndio sheria za nchi. Nguvu ya rais kuchagua kila mkuu wa chombo cha dola ndio kinachochangia rais kuteua mtu atakayemnyenyekea na sio lazima mtu mwenye uwezo. Hapa ndio nguvu ya rais kutekeleza katiba apendavyo na sio katiba na sheria zitakavyo inapopata nguvu.

Wakuu wa vyombo vya dola na taasisi za kimamlaka za umma, hupatiwa mishahara na marupurupu ya kiupendeleo ambayo hayawafanyi kufuata sheria na katiba zaidi bali ya aliyewateua ambaye ni rais ili wabaki kwenye fahari ya dunia. Kwa hiyo usitarajie CDF, IGP, C JUSTICE ama hata spika kufanya kinyume na mapenzi ya rais hata kama rais afanyacho sio. Mfano mrahisi ni hali iliyopo sasa. Nchi inaendeshwa kwa sehemu kubwa kwa tabia binafsi za rais na sio lazima sheria na katiba zitakavyo.

yule jamaa akifa shetani atamkabidh mwili wake kwa Hitler ajue cha kumfanya pale pipani

Hahaaaaa…

Una maana ya Jiwe??

Mkuu imetoa hoja za msingi sana…

Sasa wewe unapendekeza nini kifanyike ili kupunguza adha hii, kama itakuwa imeshindikana kuiondoa moja kwa moja

Very simple question The answer is LET’S BACK TO THE ROOTS ukitaka kuelewa hii nenda pale TBC maktaba waambie wakupe hotuba ya Nyerere ya 24 november 1992 akihutbia halmashauri kuu ya CCM.

Sasa wewe mwenyewe unapendekeza wapinzani waende mahakamani kupata tafsiri ya kazi ya wapinzani hapa nchini

Lakini wakati huo huo unasema kuwa Katiba imempendelea Rais kwa kumpa mamlaka ya kuteua kila Mkuu wa dola, including Chief Justice na kumjazia marupurupu mengi mno!

Vile vile unasema kuwa hao wateule wake siyo lazima achague mwenye uwezo, bali anaangalia ambaye atakuwa mpokeaji mzuri wa maagizo toka juu…

Huoni kuwa hiyo ndiyo sababu ambayo inawafanya hao wapinzani, ingawa wanajua fika kuwa wao wako "right’ katika kutekeleza majukumu yao, kuwa ndiyo sababu inayowafanya wao wasi-prefer kupeleka kesi yao mahakamani, kwa kuwa wanajua, kutokana na mfumo huo huo mbovu, kuwa kesi yao itatupwa??

Nilitarajia ungejeka na hoja hii kutokana na mchango wangu. Majibu yake yako hivi, hata kama mahakama zina pindisha sheria kwa hofu ya cheo cha rais, sio wakati wote hupindisha na hata kama wakipindisha ndio sehemu sahihi ya wananchi kujionea madhara ya rais kuwa na nguvu za ziada kunafanya mihimili mingine kama mahakama kutokutenda kwa weledi.Hii itapelekea wakati wa zoezi la katiba mpya nguvu za rais kupunguzwa kwani watu watakuwa wamejioneo kwa udhibitisho madhara ya nguvu za ziada za rais dhidi ya taasisi nyingine.

Nakupa mfano mwingine ujue wapinzani wakati mwingine na wenyewe ni pasua kichwa na wao wako kimaslahi zaidi. Hawaendi mahakamani kwa kisingizio cha kutokutendewa haki, lakini wako bungeni kila siku huku tunaona wakidhalilishwa hata wanapokuwa na hoja za msingi. Hivi majuzi tumeona bajet yao kivuli ikipigwa chini na haikusomwa, mbona hatukuwaona wamesusia bunge moja kwa moja kama kweli chombo kisichowatendea haki hawakitumii? Simply kule bungeni wanapata hela, hivyo hata kama kuna madhila wanakomaa hivyohivyo kwani wanapata hela.

Hitimisho, Hata kama mahakama zina mapungufu niliyoyataja, ndio njia pekee ya kuweza kupata haki. Na hata kama haki itapindishwa, ni sehemu ya kuweka rekodi sawa kwa faida za sheria na katiba huko mbeleni kwa kuwa mifano halisi itakuwepo.

Ana na kinga ya kifo!!!