naanza kuwamiss lumumba
mijadala kinzani ndio huchangamsha jukwaa
brainless lumumba njooni tumemiss comments za akili ndogo
Hawawezi kuja huku kwa kuwa wao ni “mercenaries” bila buku 7 hawajacomment
Uzi bora so far,kwenye jukwaa hili…wadau mmejenga hoja vizuri.
Mungu pekee ndie wa kupewa Sifa si binadam
kivyako:
Ana na kinga ya kifo!!!
Huyo Magufuli hana kinga ya kifo
Tindo:
Nilitarajia ungejeka na hoja hii kutokana na mchango wangu. Majibu yake yako hivi, hata kama mahakama zina pindisha sheria kwa hofu ya cheo cha rais, sio wakati wote hupindisha na hata kama wakipindisha ndio sehemu sahihi ya wananchi kujionea madhara ya rais kuwa na nguvu za ziada kunafanya mihimili mingine kama mahakama kutokutenda kwa weledi.Hii itapelekea wakati wa zoezi la katiba mpya nguvu za rais kupunguzwa kwani watu watakuwa wamejioneo kwa udhibitisho madhara ya nguvu za ziada za rais dhidi ya taasisi nyingine.
Nakupa mfano mwingine ujue wapinzani wakati mwingine na wenyewe ni pasua kichwa na wao wako kimaslahi zaidi. Hawaendi mahakamani kwa kisingizio cha kutokutendewa haki, lakini wako bungeni kila siku huku tunaona wakidhalilishwa hata wanapokuwa na hoja za msingi. Hivi majuzi tumeona bajet yao kivuli ikipigwa chini na haikusomwa, mbona hatukuwaona wamesusia bunge moja kwa moja kama kweli chombo kisichowatendea haki hawakitumii? Simply kule bungeni wanapata hela, hivyo hata kama kuna madhila wanakomaa hivyohivyo kwani wanapata hela.
Hitimisho, Hata kama mahakama zina mapungufu niliyoyataja, ndio njia pekee ya kuweza kupata haki. Na hata kama haki itapindishwa, ni sehemu ya kuweka rekodi sawa kwa faida za sheria na katiba huko mbeleni kwa kuwa mifano halisi itakuwepo.
Sasa kuna maana gani ya kupeleka kesi mahakamani iwapo unajua sheria zitapindishwa??
Nikuulize tu swali kidogo, hivi unafikiri ni kwanini mahakama ziliwafunga Mheshimiwa Sugu na LijuaLikali, wakati wanajua kuwa wabunge hao walikuwa wanatimiza wajibu wao kama wapinzani kwa kuikosoa serikali??