YAJAYO YANAFURAHISHA

Kuna demu mmoja kaja hapa kuomba nimkopeshe pesa nikamwambia sina cash labda bank au M pesa akanambia hapo barabarani kuna wakala twende tukatoe, wakati tunatoka nikamtext mshikaji wangu nikamwambia mi nakuja hapo kwa wakala nikifika karibu nitajifanya kama naongea na simu halafu we utakuja kunipora. Kweli tumefika karibu na wakala mshikaji kaja kanipora simu kakimbia nayo mi nikabaki nashangaa kama cjui kitu cha ajabu yule demu katoka nduki kakimbizana na mshikaji cjui kamkamatia wapi kaja anampiga makofi na jamaa yuko hoi balaaa kisha demu kanigea simu nimetoa hela nimempa kaondoka hapa mshikaji nae kaniganda nimpoze maana sio kwa vitasa alivyochezea na shati lake limechanika hata cjui nifanyeje

Hahaah noma sana

Hhhhhaaaaaaaaaaa umekomaaaa

Kkkkkkkk kudadadeki,burudika na hii nyimbo ya hisani "band nyingi zilikuja kuja na dharau zao,kudharau gari kubwa kusifia band zao…
Nalog off

Aisee

Huyo msela wako ni Mwanaume wa Dar nini?

Hao ni wanaume version ya kenya