[SIZE=5][FONT=book antiqua]Kimondo cha Mbozi[/FONT][FONT=book antiqua]
https://upload.wikimedia.org/wikipedia/sw/thumb/1/11/Kimondombozi.jpg/200px-Kimondombozi.jpg
Kimondo cha Mbozi
Anwani ya kijiografia: https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/55/WMA_button2b.png/17px-WMA_button2b.png9°06′28″S 33°02′14″E9.10778°S 33.03722°E / -9.10778; 33.03722
Kimondo cha Mbozi[1] ni kimondo ambacho kimeanguka kutoka angani karibu na mji wa Vwawa. Kinakadiriwa kuwa na uzito wa tkriban tani 16, kilianguka katika kilima cha Mlenje, wilayani Mbozi katika mkoa wa Mbeya, Tanzania.
Kipo kati ya vimondo vizito 10 vinavyojulikana duniani. Kina urefu wa mita 3.3, upana wa mita 1.63 na kimo cha mita 1.22.
Kina maumbile maalum tofauti na vimondo vingine vinavyopatikana ulimwenguni kwa kuwa hiki ni hasa cha chuma. Chuma ni 90.45%, nikeli 8,69%, sulfuri 0,01% na fosfori 0,11% ya masi yake. Ndani yake vipande vidogo vya silikati vinapatikana.[2]
Wenyeji wa eneo walijua kimondo hiki tangu muda mrefu; kilielezwa kisayansi mara ya kwanza mwaka 1930 na wakati ule hapakuwa na dalili za kasoko; kwa hiyo inawezekana ya kwamba ama kilifika kwenye uso wa Dunia kwa pembe butusana na kuvingirika hadi kukaa au muda wa kugonga uso wa dunia ni mrefi sana hadi dalili zote za kasoko alilia zilipotea tayari kutokana na mmomonyoko.[/FONT][/SIZE]
[SIZE=5][FONT=book antiqua]Source: Wikipedia. [/FONT][/SIZE]
[SIZE=5][FONT=book antiqua] https://en.wikipedia.org/wiki/Mbozi_meteorite [/FONT][/SIZE]