Dr. Evelyne Munisi aliyegombea nafasi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha NCCR Mageuzi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 amempongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuchaguliwa na wananchi kwa kura nyingi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.
Dr. Munisi amesema, Dkt. Samia alistahili ushindi huo kwa kuwa, mambo aliyoyafanya katika miaka minne ya uongozi wake yalitosha kuwaaminisha Watanzania kumpa nafasi nyingine ya kuongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.
Akizungumza na Chombo hiki cha Habari Bw. Wilson Elias aliyekuwa mgombea wa Urais kupitia chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), amempongeza Dkt. Samia Suluhu Hassan na kuahidi kumpa ushirikiano katika uongozi wake, huku akiwasihi vijana kuacha kutumika na wanasiasa kwa manufaa yao binafsi.

