Undumila kuwili wa Serikali ya Magufuli: Mbatia aende Mahakamani kushitaki Gazeti!

Nilimsikia Mbunge wa Vunjo, James Mbatia, alipoleta hoja ya Jinsi magazeti mbalimbali yalivyochapisha makala ambazo wengi wanaona ni za UCHOCHEZI na hazina tija kwa umoja wetu wa kitaifa. Jana Waziri Mwakyembe tumemsikia akimjibu Mbatia, kwamba ameshitushwa na kauli za “uwepo wa ubaguzi wa kikabila” kuletwa bungeni, kwamba hapa si mahali pake, kwamba kama anaona kabila la wachaga linabaguliwa basi aende mahakamani. Mwakyembe alijaribu kuhamisha msingi wa mada kutoka tishio kwa umoja wa kitaifa kuja kuwa ni tishio kwa mtu au kikundi, na akasema ufumbuzi ni kwenda Mahakamani.

Serikali ya awamu ya Tano inaonekana imegundua mbinu ya kukabiliana na tuhuma na mashambulizi mbalimbali kutoka kwa WAPINZANI, nayo ni “kuwashauri” waende mahakamani kufungua kesi. kuanzia shutuma za kuvunja katiba ya Jamhuri ya Muungano, na pia Sheria ya Vyama vingi, kwa kuzuia mikutano ya siasa, kubana magazeti na vyombo vya habari na mitandao, mpaka hii iliyoletwa bungeni na Mheshimiwa Mbatia, ushauri ni huo huo: kama mtu anaona kwamba hajatendewa haki, aende mahakamani!

Ukiangalia juu juu utakubaliana na akina George Mkuchika na Mwakyembe, kwamba kwenda Mahakamani si ndio kwenye utoaji wa haki? lakini ukichunguza kwa makini utagundua kwamba kuna hila ipo ndani yake. Kwanza kabisa, pale inapotokea kwamba Serikali yenyewe imekosolewa vikali, au kikundi cha watu au mtu au taasisi yenye msimamo unaounga mkono ule wa Serikali, basi Serikali wala haiendi mahakamani, na wala haisubiri huyo mtu au kikundi au taasisi inayounga mkono serikali, waende mahakamani. Serikali huchukua hatua yenyewe, ama kufungia kama ni chombo, au kumtetemesha huyo mhusika kwa “kuhojiwa na Polisi” tena kwa ratiba ya kumchosha. mara ngapi serikali imefungia magazeti yenye msimamo unaotofautiana na wa serikali? tena kwa hoja dhaifu? pia wakati Kardinali Pengo alipotofautiana na Maaskofu wenzake kuhusu waraka fulani ulitolewa hapo nyuma, siyo huu wa juzi wa Kwaresima ya 2018, Askofu Gwajima alimshambulia na kumkosoa. Serikali badala ya kusubiri Kardinali Pengo aende mahakamani kufungua kesi, Jamhuri yenyewe ilifungua kesi dhidi ya Gwajima, na alihojiwa na Polisi hadi presha ilipanda ikabidi apelekwe Hospitali kwanza.

Lakini kwa hili la “waraka dhidi ya Kanisa Katoliki” kuchapishwa na magazeti, tena huo “waraka” ni wa kichochezi haswa, Serikali inakaa pembeni na kudai kwamba kama kuna mtu anaona hajatendewa haki, aende tu Mahakamani!! Kuna suala la huyu mtu anaitwa Musiba, ambaye anatoa tuhuma nzito na vitisho na hata kutishia vifo kwa wanasiasa wa upinzani. lakini kwa kuwa wanaoshambuliwa ni “WAPINZANI”, ambao kwa mujibu wa serikali yetu, WAPINZANI siyo WATANZANIA, basi serikali iko kimyaaaa, utadhania haipo vile. ukitaka kujua kwamba nchi hii kuna serikali, mchokonoe Magufuli, au serikali yenyewe, hapo utajua.

Mheshimiwa Mwakyembe, tumekusikia, na wala hujatudanganya. unajidanganya mwenyewe na serikali yenu ya kikandamizaji na undumila kuwili.

Upuuzi umejaa sana nchi hii

Huyu bora ile sumu ingemuua kabisa kwani hana faida yoyote tena hapa duniani.

Tatizo ni kwamba serikali nzima inasubiri maelekezo ya mtu mmoja tu, na hilo Ndugai kadhibitisha jana wakati anawatishia wabunge kuhusu bajeti.

!
!
Mhimili Uliojichimbia Zaidi Ni Shida Sana.

huyu musiba analelewa sana

Haya ni mambo ya ukabila ni mazito sana. Bila shaka kauli iliyotoka bungeni itakuwa imemfanya Baba wa Taifa ageuke ndani ya kaburi lake! Kupiga vita ukabila sasa ni siyo kazi ya kisiasa na kijamii bali ya kisheria? And this from a Ph.D? Methinks kuna siku kama taifa tutakuja kakaa chini na kutafakari kwa kina mambo haya.

Huko mahakamani wanajua mtakutana na hao hao

Halafu mshenzi eti ana PHD. Mamaeeee zake. Hatuna waziri pale. Tuna mabaki ya sumu tuu yanamtafuna mwilini.

Huyu wala syo sumu, kilichomuua mkewe ndicho kinachonsumbua,kaleta gonjwa nyumbani kasababisha mkewe kufa,gonjwa limemharibu hadi ubongo sasa anaweweseka kama mwendakuzimu

Wala hajakosea huyu maana ugonjwa umemharibu ubongo kila anachoambiwa na sisonje anapokea kama zuzu.swala la ukabila ameliasisi kwa maneno na matendo mpendwa wetu rahisi, hili haliishi hivihivi maana tz syo ya wasukuma pekee miaka saba ilobaki sii mingi nchi atatawala mtu toka mahali popote na kabila lolote bila kusahau 2020 tutahubiri ukabila ktk kampeni,misikitini hadi makanisani, maofisini hadi ktk familia, mpuuzi huyu hatuwezi kumuacha aendekeze ujinga na ushamba wa gambushi

Sasa ukishaenda mahakamani, kwanza watahakikisha wanakukwamisha kwa njia mbalimbali. Serikali za nyuma walikuwa hawaingilii sana mahakama. Hii awamu achana nayo kabisa. kesi nyingi wanazofungua CHADEMA, kama ile ya rufaa ya Sugu, iliishia danadana ya kutopangiwa jaji mpaka Sugu katoka kwa “msamaha”. Lakini pia ukishapeleka shauri mahakamani, ndio huruhusiwi tena kuliongelea popote, siyo bungeni siyo wapi. ukitamka tu wanakuambia shauri liko mahakamani hutakiwi kuliongelea. ndio ushapigwa kufuli la Magufuli.

Bora mtu awe mpuuzi ambaye hajasoma tutamsamehe sasa inapotokea msomi wa ngazi ya udaktari naye anafanya mapuuza huyo sasa ni wa kumuweka karibu na wodi ya vichaa just in case!

Mbona Mwakyembe aliyafungia magazeti bila kuyashitaki mahakamani? Haya mbona anajiuma-uma?

Kaka

Hakuna hakimu atakayesimamia hiyo kesi, mtapigwa kalenda weee, kwa maagizo kutoka juu

Exactly

Watapata tabu sana! Serikali ina double standard kweli kweli…lakini ni wazi itapotezwa na wote wanaotenda hizi dhambi watapata tabu sana!

Na siku huyu waziri akifa tutasema taifa limepata pigo!!!

Serikali ni watu, na watu wenyewe ndio JIWE

Nimeeleweka?

Naunga mkono hoja, pia nna mashaka na hizi Dr zao