Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 06 Februari, 2018 amezindua Kituo cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi (Comprehensive Training Center – CTC) kilichopo Mapinga katika Wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani. Kituo hicho kimejengwa kwa msaada kutoka Jeshi la Ukombozi la Watu wa China kwa gharama ya Shilingi Bilioni 67.87 na kitatumika kutoa mafunzo ya kijeshi ya kisasa yatakayowawezesha askari kukabiliana na vitisho vya kisasa vya kiusalama.Mhe. Rais Magufuli amelishukuru Jeshi la Ukombozi la Watu wa China na Serikali ya China kwa kutoa msaada wa kujengwa kwa kituo hicho na amesema Serikali ya Awamu ya Tano inathamini na kutambua mchango wa China katika Jeshi la Ulinzi la wananchi wa Tanzania. Mhe. Rais Magufuli amesema China imeendelea kudhihirisha urafiki na udugu wake na Tanzania kwani licha ya kujenga kituo hicho pia imetoa msaada wa kujenga kituo cha mafunzo ya kijeshi ya anga cha Ngerengere Mkoani Morogoro na miradi mingine ya maendeleo ya jamii na hivyo amemuomba Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke kufikisha shukrani zake kwa Rais wa China Mhe. Xi Jinping.
https://3.bp.blogspot.com/-ozFRR-omX_A/Wnm1sPdU_KI/AAAAAAACKmw/pGXdGuuS_6Y4uZwK9Ohsz9JGmZ1hIBmmgCLcBGAs/s640/10.jpg
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe
Magufuli akiagana na Naibu Mkuu wa Idara ya Usimamizi wa Mafunzo kutoka tume Kuu ya
Kijeshi ya China Meja Jenerali Yang Jian mara baada ya kukifungua kituo hicho cha Mafunzo Maalum ya Kijeshi.
we will still subsidize our blue band exports you you ujamaa beggars
is it something to be proud of to be begging the chinese like we dont have brains in our heads…this is shameful and yet you post it as if tanzania achieved something. what an inferiority complex!!!
Post kwa blog za TZ
Magufuli in his elements, as usual.
It is preferable to comb all nook, granny and crack of the buildings to insure Chinaman bugs were not secretly installed by sly, covert chinese builders.