Nina swali dogo kuhusu uzalendo wa ukimbizini na ugenini.
Inapotokea, baba yako akiwa mlevi, karudi, kajitapikia sebuleni na kampiga mama kwa kisa mama kamwita mlevi, na ulipoamka asubuhi ukawasikia baba na mama wanazozana chumbani kuwa saiti, mama akigomba, kwa kwa nini ujikolee kitandani?, hatuna mtoto mdogo, tukianika godoro nje, majirani watatuonaje?, wewe mtoto ulishuhudia baba akijitapikia, ulisikia baba akiitwa mlevi na kushuhudia kipigo kwa mama, kesho yake asubuhi ukashuhudia godoro likitolewa kuanikwa uwani, wewe unapokwenda shule. huko barabarani na mitaani jee utahadithia tuu kuwa baba ni mlevi na jana kajitapikia, kampiga mama, na usiku kajikojolea kitandani?!, au utajinyamazia kwa kusikitika, kuhuzunika na kutahayari kwa hali ya nyumbani, kuficha aibu ya baba na matezo ya mama?.
Mambo mengine ni aibu, tuyaache na kuyahifadhi kama siri za ndani, ikibidi kumsitiri baba yetu, japo kweli ni mlevi, lakini kwa huku nje, ugenini, tumsitiri kisha nyumbani ndipo tubanane nae ili majirani wasijue aibu za baba yako, na mateso ya mama yako?.
Uzalendo wa kweli wa nchi yako jee sio ni pamoja na kuficha siri zetu za ndani?.
Jee kwa jinsi watu wanavyomtukana Baba nwenye nyumba huku ugenini, japo ni kweli, lakini ni haki kweli?, ni uzalendo?.
Kwanza sikutegemea na wewe utakuja huku baada ya likizo uliyojipa kule JF, Huku tutaendelea kuanika magodoro na chupi zetu maana haya amejitakia mwenyewe chafu barazani. Baba akiwa mlevi hiyo ni aibu yake yeye binafsi hainigusi mm. kwa hatua tuliyofikia ni bora zigo la lawama limwendee baba peke yake
paskali kwanza pole kwa mkwala uliopitia, lkn kumsema baba kwa jirani inaweza kuwa dawa ya yy kutorudia madhambi yake,ona katuziba midomo sasa tunasemea wapi? kwa hiyo anafanya haya makusudi siyo? kwa kuwa anauwezo wa kuita malaika wafunge mitandao siyo ila anaudhi sana ila basi tu.
Ni siku za karibuni tu tuliwazika wapendwa wetu Maria na Consolata,mapacha walioungana. Wailukwa walemavu. Tulishauriwa tusiwafiche walemavu ndani,tuwatoe kwenye jamii ili kwa pamoja tushirikiane kuwahudumia.
Huku ndio mahali pazuri kwa kuweka udhalimu wote hadharani. Hata huko nyumbani tulikuwa tunatumia online platforms ambazo zinaonekana dunia nzima. Cha muhimu ni kusema ukweli.
Niliposoma kichwa cha habari nikaona nisiendelee na jibu lake ni kama ifuatavyo
Baba akizidi kuwa muhuni ndani ya familia sometimes hata kichapo aweza kupata…usinihoji kuhusu hili…Biblia imeandika Enyi wazazi msiwachokoze watoto wenu…
Maana ya Neno hili ni kwamba, watoto ni wanadamu na wananyama kama Baba na wahisi maumivu yoyote watendewayo…
Kifupi nikwamba huu sio mda tena wakumbembeleza JIWE…kama mbaya wacha iwe mbaya.
Binafsi sitasubiri mboga ifike mezani nitamwaga.
acha baba asulubiwe, watoto hawana maji safi wala madawa yeye ananunua SUV la bei mbaya ili akajitape bar mbele ya walevi wenzake. alafu bila aibu anajitapa mbele yetu “fahari ya familia ni SUV”