Kwa wale ambao hawajasikia, jana mh, peter selukamba, akitoa hoja bungeni ili wajadili wale maafisa w Maliasili walioenda kwenye kantini za bunge kupima samaki kwa rula wakiwa hawana kibari chochote cha bunge
Baada ya mjadala spika alitoa maelekezo kwa waziri mkuu akete majib ni kwa nn hao maafisaa walikija kwenye kantini ya bunge
Kuweka kumbukumbu sawa, kumekuwa na malalamiko ya mda sasa kwenye wizara ya uvuvi juu ya ukatwazaji wa samaki, na kunakipindi mbunge MSUKUMA,. wa jimbo la GEITA VIJIJINI, alitoa malalamiko hayo
Kumekuwa na malalamiko mengi juu ya wananchi kwa maafisaa wa maliasili kuwa nyanyasa wananchi wanaovua au wanapata kitoeo, nakukisafirisha,
Wakati fulani gari la mbunge(msukuma)
Lilikamatwa likiwa na mteja aliebeba samaki na kuamuliwa kulipa faini ya m.3,
Mwenye taarifa zaidi atuwekee kwa nn samaki imekuwa kama madawa ya kulevya?
Mkuu me nipo huku zinakotoka wenyewe wanaita mwaloni yaani ni balaah wababa wametelekeza familia zao haijulikani lini wanarudi maana hata hewani hawapatikani, kwenye daladala za huku ni kama wimbo makondakta wanavyokomalia watu wasinunue wala kupakia Samaki kwenye magali Yao.
Hii imekuwa vita zaidi ya madawa mkuu
Samaki ni haramu kuwa nae mkononi.
Hili la maafisa uvuvi kikosa vifaa sahihi vya kukagua samaki na badala yake kutumia vifaa vya mashuleni/stationery limenikera. Pia wameenda kwenye sahani badala ya pwani (fish landing station).
Kaazi kweli kweli. Mi yangu macho na masikio tu nikifuatilia hizi dakika za kipindi cha kwanza zitakuwa na matokeo gani kwenye mchezo huu unaoitwa awamu ya v
Kaazi kweli kweli. Mi yangu macho na masikio tu nikifuatilia hizi dakika za kipindi cha kwanza zitakuwa na matokeo gani kwenye mchezo huu unaoitwa awamu ya v