Nisiwe ' mwongo ' jamani huku tuliko ' Ukimbizini ' wala hakunogi kama kule ' Nyumbani ' tulikokuwa

[FONT=courier new]Uwepo huku KT hauna tofauti na Mwanaume kukimbiwa au kuachana au kuachwa na Mpenzi / Mke wako ambaye ulimpenda kweli ila kwakuwa tu hakuna namna na Wewe ni Mwanaume unahitaji kutimiza haja yako ya Kirijali na Kibaiolojia basi inakubidi tu ufanye ’ tendo ’ hilo hata na Mwanamke ambaye hujampenda au humpendi.

Ninamlaani sana aliyetusababishia huu ’ usumbufu ’ mkubwa Sisi Watanzania Wanyonge ambao tuliuzoea, tuliupenda na tuliuamini sana Mtandao wetu ’ pendwa ’ wa JamiiForums. Kwa hizi wiki mbili tu sasa kutokuwepo kwa Mtandao wa JamiiForums nchini Tanzania kwa sasa naona nimepoteza ’ maarifa ’ mengi na makubwa sana.

Ni ’ madini ’ ya uhakika ambayo nilikuwa nikiyapata ndani ya JamiiForums ndiyo yalikuwa yakinifanya niwe ’ Kijana ’ ninayeaminika na kukubalika mno na Wanajamii wengi maeneo mbalimbali tena na Watu wa ’ rika ’ zote na kulikuwa na uelekeo ambao nilikuwa nikiuona kabisa Kwangu wa kwa jinsi nilivyokubalika na Wanajamii eneo ninaloishi kulikuwa na uwezekano mkubwa mwaka 2020 nikamvua Mtu ’ Jimbo ’ lake la ’ Ubunge ’ ili nami kuanzia mwaka 2020 jina langu libadilike katika kuitwa Mkuu GENTAMYCINE sasa niwe naitwa Mheshimiwa GENTAMYCINE na kwa ’ Uadilifu ’ wangu, umakini na uchapakazi nina uhakika hata katika ’ Cabinet ’ la 2020 ningekuwa ama Naibu Waziri au hata Waziri kamili katika ’ docket ’ fulani ndani ya Serikali ya Tanzania.

Nitaililia na kuimbuka sana JamiiForums kwani sina raha tena japo tumekaribishwa huku ’ Ukimbizini ’ lakini tusisahau kwamba hata iweje au itokee nini Nyumbani ni Nyumbani tu. Huku ’ Ukimbizini ’ Watu ’ tunadanganyana ’ mara wengine wanaiba ID’s za Watu na wanajifanya ni Wao, wale Watu makini ’ Werevu ’ huku tulipo sasa ni wa kuwatafuta kwa ’ tochi ', ule mvuto wa majibizano ya ’ Hoja ’ kama kule JamiiForums huku haupo yaani mambo ni ’ vululu vululu ’ tupu!

Furaha yangu ya 100% itarejea / itarudi tu pale Mtandao wa JamiiForums utakaporejea na kuendelea kutoa huduma zake kama awali.

Nawasilisha.[/FONT]

bwana ametoa na bwana ametwaa, jina lake lihimidiwe, JF tulimpenda ila TCRA walimchukia zaidi

We acha tu ndugu, labda tutazoea si unajua new villager tena! Lazima maisha ya kijijini yawe magumu kwa muda. Hope tutazoea maana kule town nako Mh!

wale wakimbizi wakisiasa wangeondoka na Melo bado tungekua tunapeta mpaka sasa, nje kwa nje live. Mipango haikuandaliwa pamoja na dalili zote za wazi juu ya kifo cha Jf.

Information za kuanzia 2006 mpaka sasa ni hazina kubwa sana. Hakuna kitu utatafuta ukakiosa JF. Hope itarudi siku za karibuni.

Kweli kabisa…

Nina miss sana zile habari moto moto kila dakika chache,huku unakaa siku nzima no beaking news ! wacha tu tuvumilie…

MUNGU IBARIKI JAMII FORUM

Imerudi mbona.

Aisee

TCRA wana balaa.

Kwakweli huku pamepoa sana jf ilikuwa moto sana.

Nimeshindwa kupazoea, nilidhani ni mimi tu, yaani humu sichukui hata nusu saa nasepa

Acha u

Acha urongo mkuu

Nikweli ila mwanzo mgumu siku zote

hakunogi ila hakuna jinsi

Wala sio uwongo kila nikiingia nashangaa shangaa tu daaa huyu Mungu mtu basi tu

Upo bongo au nje?

H

Hata huko nje aijarudi

Sasa huyu jamaa mbona anapotosha??