Leo baba katika kikao na wanahabari amesema anaunga mkono vile wabunge walivyopiga firimbi jana wakati wa hotuba ya rais.
Hivyo basi, sina budi kuomba msamaha kwa wanachama hususan Opiyo Wandayi, Gladys Wanga, John Mbadi, Kajwang na Millie Odhiambo kwa vile nilivyowakashifu jana usiku.
Nina kero moyoni kwa kutounga msimamo wa chama. Nimeletea familia yangu aibu kwa kutokiuka msimamo wa chama. Natumai wanachama watanisamehe na wanikubali ili niendelee kujitolea kimawazo na kifedha kunufaisha chama iliyo nambari mbili Afrika katika demokrasia nyuma ya ANC.
Swali ni, kama kweli swala hili ilikuwa msimamo wa chama, mbona wabunge wengine wenzenu hawakuondoka bungeni spika alipoamuru kuwa asiyetaka kuskiza hotuba ya raisi alikuwa amepewa nafasi ya kuondoka