Huyu jamaa aliwahi kusema kwamba iko siku hawa jamaa watatwambia tuwabong,olee kama tutaendelea kuwachekea. Leo maneno yake yametimia kwa msaada alioutoa yeye mwenyewe kwa kukipigia Kampeni chama cha wahuni kuingia tena madarakani kwa njia haramu alizosema kwamba ilikuwa haina namna kwa kuwa CHADEMA walikosea kumsimamisha Lowassa badala ya Slaa.
haha asante nimekaribia , Mwanakijiji alisahau ngano ya “Mtego wa Panya”,Panya aliwatahadharisha kina panya,mbwa,ng’ombe wamsaidie kuutegua mtego wa panya maana haukumlenga yeye panya tu peke yake wakiuacha hata wao na wenyewe utakuja kuwadhuru lakini hawakusikia,mwache mwana kijiji asome namba.
Allen mbona hukumwelewa mzee mwanakijiji. Watu wenye ufinyu wa maarifa bado wanafikiri kuwa Lowasa angeshinda urais. Chadema walifanya maamuzi ya hovyo kumkumbatia Lowasa badala ya Dr Slaa. Na haitakuja kutokea Chadema wakatawala nchi hii, labda Tundu Lisu aongoze chama hicho.