Mh.Nape Nnauye:"Nilaumuni kwa bao la mkono si kwa hili la JF"

Mh Nape Nnauye,Mbunge wa jimbo la Mtama na aliyekua waziri wa Habari,Utamaduni na Michezo na aliyempigia kampeni dikteta Magufuli ameandika kwenye ukurasa wake wa twitter kuwa tumlaumu kwa bao la mkono lakini si kwa hili la JF,inaonyesha kuwa hata Mh.Nape na baadhi ya makada wa CCM wengi hawafurahishwi na hatua ya kuifunguia JF.

Kwani nayeye ameshakuja huku ‘‘diaspora’’ ? Maana najua kule ''nyumbani" nayeye alikua mwanachama. Tuanzie hapo

Hivi huku kuna app kama kule kwetu.

Yote yeye kafanikisha.

Alifanikisa bao la mkono, akaja kufanikisha kupitisha sheria kandamizi za mitandao alipokuwa Waziri.

Lawama hizi hachomoki hata kidogo

Hamna App mkuu.

Komaa tu web, tumejaribu kuwaomba watengeneze App sijui kama watakubali

Nafsi inamsuta, alikuwa anafanya kumfurahisha malaika lakini amekuja gundua kuwa hakuwatendea haki raia wa Tanzania pamoja na vizazi vyake na yeye akiwemo ndani. As a human amejiona yuko guilty

hawezi kukimbia yeye ndio mhusika no 1

Nape ni kama yule rubani aliyedondosha Bomu la hiroshima…

NAPE…ANATAPA TAPA TUUU

Nape mpaka utawala huu uishe atakuwa kaziona rangi zote,jamaa ana maumivu makubwa mno na aangalie alishaoneshwa mpaka mguu wa kuku

Kweli kabisa aise Ndugu.

Anajifanya ana uchungu kwa yanayoendelea kumbe mnafiki tu, nafurahi huko Twitter hawajamkawiza, kajifanya kujitetea kuna mdau kampa kubwa kuwa baada ya mswada wake kupita alifanya mpaka sherehe, jamaa hafai hata kurumangia na dona.

anakwepa lawama

Akitubu toka moyoni labda atasamehewa hii dhambi.

mkuu hii avatar yako nilikua natumia kule jf sasa hum nimeona nibadilishe maana japo ujumbe ule ule

Wana siasa bwana.

Ata Mimi nilikuwa naishangaa Sana account yako kuwa na avatar…kama yangu…Mimi account zangu zote Zina avatar hiyo.

Roho inamsuta sana

Hahah! Eti dikteta uchwara

FISIEM ni FISIEM tu