Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akichangia
Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde akichangia mjadala wa kupitisha Bajeti Kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2018/2019, jijini Dodoma leo. Picha na Edwin Mjwahuzi
Kwa ufupi
Ametoa kauli hiyo leo bungeni mjini Dodoma
By Ibrahim Yamola, Mwananchi [email protected]
Dodoma. Livingstone Lusinde amewapiga marufuku wabunge wa CCM kukikosoa chama hicho tawala ndani ya Bunge.
Mbunge huyo wa Mtera (CCM) ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Juni 25, 2018 katika mjadala wa bajeti ya Serikali mwaka 2018/19, kusisitiza kuwa yeye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho.
“Humu ndani tunapochangia tujiepushe na kazi za wengine. Eti tukifanya hivi tutashindwa sisi si wasemaji wa chama. Sisi wabunge wa CCM kazi yetu ni kuisimamia Serikali, kukosoa na kuitetea na nasema kama bosi wenu humu ndani ni marufuku kwa mbunge wa CCM kukizungumzia chama humu,” amesema.
“Hiki ni chama chenye Serikali na tupo hapa kuisimamia si kuikosoa CCM. Chama kushinda au kushindwa si sehemu yake hapa. Kama wabunge wangu hamna lugha ya kuisifia na kuikosoa tulieni.”
Kuhusu mvutano wa korosho amesema, “Humu ndani kuna wanasheria wengi, hivi wanashindwa nini kulitolea ufafanuzi hili la korosho likaisha. Sioni haja ya kutukanana katika hili.”
Sasa mbona una mtukana wakati mwenzio kaweka bayana hoja zake? ulisha waona wana chadema wanaikosoa chadema bungeni? kosa la lusinde ni lipi? Mimi nafikiri wewe ndiye “taahira” kwa mwendo huu ikulu mtaisikia tuu kwenye bomba
Jamaa ni mpumbavu sana hajui hata wajibu wa Wabunge ni upi. Kwa akili zake finyu huyu taahira anadhani yuko Bungeni kuipigia debe Serikali na kuitetea kwenye maovu na madudu yake.
Waikosoe Chadema kwani ndiyo iliyo unda serikali? mbona wewe huwa una akili za kizoba hivi? kazi ya wabunge wanao wakilisha wananchi ni kuikosoa serikali iliyoko madarakani, na kwa hilo ccm iliyo unda serikali hiyo haina pa kutokea na hata wabunge wa ccm wanayo haki ya kukosoa