Kwa wale wanaojua Magufuli anaipeleka wapi nchi? Na wanao muunga mkono watuambie KWA NINI ANAOGOPA/HAPENDI KUKOSOLEWA AU KUPINGWA?

Magufuli aliingia madarakani kwa AHADI kubwa zifuatazo.

  • kupiga vita RUSHWA na matumizi mabaya ya madaraka.
  • kupiga vita uzembe na kutowajibika kwa watumishi wa uma.
  • kuwaletea maendeleo ya haraka wananchi hasa wanyonge.
  • kuboresha elimu na masilahi ya wanyakazi
  • kuondoa UMASIKINI, MAGONJWA, UJINGA na UFISADI.
  • kuifanya TANZANIA YA VIWANDA.

BAADA YA TAKRIBANI MIEZI SITA TU YA UONGOZI WAKE
VITA IKABAFILIKA IKAWA DHIDI YA

  • kupambana na vyama vya SIASA
  • kuua uhuru wa vyombo vya habari
  • kungoa meno ya bunge
  • kuleta hofu kubwa ya kutekwa, kupigwa risasi nk
  • kuvunja katiba
  • kupambana na yeyote mwenye mawazo mbadala na yeye
  • kuigawa nchi kichama na kikanda.

KUNA MAMBO ANAFANYA VIZURI SANA LAKINI UHURU KWANGU NI MUHIMU KULIKO KITU KINGINE CHOCHOTE. Ndio maana tulidai UHURU wetu kutoka kwa wakoloni pamoja na kwamba walitufanyia mambo mengi.

Usishindane namimi,halafu nitawafungia hata huku,acheni kuleta uchochezi.

Haaaaahaaaaaa.Eti nitawafungia hata huko. Huwezi wewe.

Jinga.

Tufungie

ni woga wake tu kwa nini usipende kukosolewa serikali yoyoyote ile lazimz ikosolewe ywyw anataka asifiwe tu hata kama anafanya mabaya

Tabia yake bila shaka inatokana na malezi yake. Mtoto akilelewa kwenye mazingira ambayo anakosolewa vikali na kupewa adhabu nyingi kila mara mwisho wa siku anaishia kuwa mtu asiye jiamini. Akiwa mtu mzima basi hujihisi ni mtu mwenye mapungufu mengi ambayo hangependa wengine wayaone hivyo hujitahidi kuishi maisha ya kuigiza ili kuficha yale mapungufu anayohisi kuwanayo. Lakini akipata power, basi njia hubadilika na mtu wa aina hiyo hataki kusikia ukosoaji wowote ambao anaona ni kama unayaanika yale mapungufu yake. Atatumia power kuhakikisha anakua na picha safi mbele ya jamii kwa kuwapoteza wakosoaji wote. Yeye huishia kuwa dikteta

Mzee mchoyo huyo,hapendi maendeo ya wenzake…

Ana roho ngumu sana utadhani ataishi milele

Aliingia kwa mbwembwe nyingi za nchi kujitegemea na kuwa donor country yaan waliopita wote walikuwa wanakosea na hawafai…kilichotokea ye ndio amaeirudisha nchi nyuma kwa kila kitu.

uongozi sio mchezo mkuu ,kuongoza nchi si sawa na kuongoza familia!

lakini gia ikabadilishwa angani na sasa mambo ni juu chini ,chini juu mpaka wengine tumeomba hifadhi ya ukimbizi kwa muda kwa ndugu zetu wakenya !

usitutishe ewe jiwe kuu!

ubavu huo hana !

Watu wasiojiamini ndio walivyo…mkuu habari za siku

Dictators are always cowards, muone shost wake Kagame anavyomuogopa demu Diana Rwigala, dikteta wetu yeye anaiogopa mitandao

Huyu ni kichaa tu.

Nafarijika sana kuwaona wakuu munajaa pande hizi, bila shaka TCRA Boss wao wanakuna vichwa nini kifuate.

Aisee hata Mimi nafarijika sana kuwakuta huku wadai jf, hakika sasa ile atosto ya jf imepungua, tcra hawana akili maana huwezi kuziba watu midomo wasiseme, ukiwaziba lazima watafute mahala pengine pa kusemea

nchi imeuzwa