TUNAIGIZA MAISHA YA KIJAMAA KWENYE TANZANIA YA KIBEPARI.
Habari great thinkers,
Kwanza poleni wana JF wote ambao tyumefanyika kuwa wakimbizi wa kimtandao, Mimi ni mkimbizi mwenzenu ninayeishi uhamishoni nchini kenya kimtandao. nikienda moja kwa moja kwenye mada yenye kichwa tajwa hapo juu, nadhani aina ya social-political formation ambayo tunaifata Tanzania nayo ni kikwazo katika kutufikisha mahala ambapo ni bora zaidi ukilinganisha na tulipotoka.
Aina ya social-political formation ambayo tunaifata Tanzania nashindwa kuielewa hadi leo maana yake kwenye katiba tunaambiwa kwamba Tanzania ni nchi ya kijamaa lakini kiuhalisia sisi tunafuata ubepari. Sheria nyingi za Tanzania zingefaa zaidi kama tungekuwa ni wajamaa pure lakini zinaonekana kuwa hazifai na kandamizi kwa sababu zinaongoza nchi ya kibepari, nitatoa mifano michache
- Hivi karibuni serikali iliweka figisu figisu kwa Klabu ya soka ya SIMBA ili[potaka kumpatia mwekezaji asilimia 51 za hisa za klabu ili awe na final say kwa mambo yanayohusu klabu, hili liligonga mwamba baada ya Waziri mwenye dhamana ya michezo kuwazuia kwa kuwa sheria hairuhusu mtu mmoja kupewa zaidi ya 49%, hii inaonyesha wazi kwamba jinsi serikali na sheria zake zinavyo discourage private ownership na maendeleo kwa ujumla katika soka kwa sababu tunaigiza maisha ya kijamma kwenye Tanzania ya kibepari.
- Sakata la mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu, Tanzania ukisomea shule binafsi ni kosa la jinai na hupaswi kupatiwa mkopo (mimi mwenyewe ni victim wa hii inshu maana nimeomba mkopo mara 3 mfululizo na nimenyimwa kwa sababu form 5 na 6 nimesoma private na mara zote sababu za kuninyima ni kwamba nimesomea A-level shule binafsi)
Hizi ni baadhi tu ya mifano halisi ambayo nimepata muda wa ku share nanyi ndugu zangu kutokana na muda nitaishia hapa na nitaendelea ku update kila nipatapo muda, nanyi ndugu zangu mnaweza kujazia jazia hapo.
WASALAAM, Mwanachama mnazi wa JF