Ndugu zetu wakenya msikereke kwa kuona ghafla kwenye nchi yenu (Kenyatalk) kiswahili kimetamalaki. Waswahili tuliokuja huku hatukuja kwa mapenzi yetu bali tupo ukimbizini na kiswahili mnachokiona hakizungumzwi kwenye miji yenu (Kenya Forums) bali kinazungumza ndani ya makambi yetu ya wakimbizi.
Bahati tuliyonayo wenzenu ni kwamba Kiingereza cha kubabia tunacho na kiswahili tunacheza nacho kama mwanasesere mikononi mwetu, nyie wenzetu Kiswahili kwenu ni Pasua Kichwa. Vumilieni tu kwani wakimbizi huja na mila na tamaduni za kwao!
Issue ni kivumiliana, having an open mind and learning from each other. No one has exclusive rights to any language and we must appreciate that all languages are dynamic and take variations in different regions.