JINSI RAISI MAGUFULI ANAVYOLIISHI AZIMIO LA ARUSHA (1967)

Azimio La Arusha (1967) ni tamko rasmi la Serikali kuhusu Nchi itakavyoendeshwa kwa kutumia siasa ya ujamaa.na kujitegemea.

Kila mpenda usawa,haki, maendeleo anapaswa kuunga mkono jitihada zinazofanya na Rais JPM ambazo ziko wazi hazihitaji nguvu ya ziada kuonekana.

Kwa nchi yetu ilipokua imefikia ilihitaji mtu mwenye nia ya dhati na moyo wa kizalendo na uadilifu mkubwa ili kuitoa ilipokua na kuisogeza mbele kimaendeleo.

Raisi Magufuli imeonekana kuwa serikali yake inaenda sawia na azimio la ambalo lilikua na sehemu tano ikiwa ni,1.Itikadi ya chama cha Tanu, 2.siasa ya ujamaa, 3.siasa ya kujitegemea, 4.uanachama wa TANU na 5.Azimio la Arusha

Na kwa mwananchi anayejua yaliyomo katika azimio hilo ni wazi kuwa angependa kuongozwa na kiongozi anayeweza kuliishi pamoja na misingi yake.
Serikali ya Raisi Magufuli imeonyesha baadhi ya vitendo vilivyo ndani ya Azimio hilo ikiwepo,

Mapambano ya vita vya kiuchumi ikiwa ni moja ya ahadi alizotoa wakati wa kampeni zake za Urais mwaka 2015.

Mwalimu Nyerere alisema katika mapambano ya vita vya kiuchumi Mwalimu Nyerere alisema “Tumeonewa kiasi cha kutosha, Tumenyonywa kiasi cha kutosha na Tumepuuzwa kiasi cha kutosha. Unyonge wetu ndiyo uliotufanya tuonewe, tunyonywe na kupuuzwa. Sasa tunataka Mapinduzi, mapinduzi ya kuondoa unyonge ili tusionewe, tusinyonywe tena wala tusipuuzwe tena”.

Na hiki ndicho Rais Magufuli amekua akikifanya mara kwa mara kupigania uchumi wetu ili tusioendelee kunyonywa

Pia tatizo la ufisadi Rais Magufuli amelishughulikia ipasavyo ambapo imeanzishwa mahakama ya mafisadi kwa ajili ya kushughulikia wabadhilifu wa uchumi

Pia fursa ya Elimu Bure ni kitu kilichodhihirisha namna Rais Magufuli anavyo tembea na Azimio la Arusha, ambapo azimio lilisisitiza kuwa maarifa ni nyenzo ya pili ya maendeleo yakitumika sambamba na juhudi. kwa kutambua hilo Serikali imetoa fursa kwa kuwawezesha watanzania maskini kupata elimu bure kuanzia Elimu ya Awali hadi kidato cha nne.

Ulipaji wa kodi, ni kati ya vipaumbele vinavyosisitizwa na serikali ya Dk. JPM juu ya kila Raia anayestahili kulipa kodi kufanya hivyo kwa ajili ya maendeleo ya Taifa.

Na matumizi ya lugha yetu ya Kiswahili. ni kipaumbele ambacho Raisi Magufuli anaonyesha dhahiri dhana ya kuenenda na Azimio la Arusha. Ambapo Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kushirikiana na Baraza la kiswahili la Taifa (BAKITA) nao hawako nyuma katika hili la kuchochea matumizi ya Kiswahili kwenye nyenzo ya kuunganisha watanzania na kueneza Kimataifa.

#Tanzaniayetumpya
#uzalendokwanza

[ATTACH=full]177962[/ATTACH]

Wapiga Zumari wa mfalme

Kama anafata Azimio la Arusha well, BUT haiondoi tabia zake MBAYA na za OVYO za KIKATILI kama kumpiga Lissu risasi, kuteka na kutesa, kukandamiza wapinzani, kukandamiza Demokrasia na Uhuru wa kujieleza, kufungia magazeti nk nk.

Huyu hata afanye jambo njema gani, haya hapa juu ndio ALAMA yake kuu.

lakini hauna uhakika na haya unayoyasema, unafanya guess work. ambapo vile vile waliompiga risasi Lissu what uf ni wenzake wanaomuonea gele labda ili mwingine achukue nafasi yake alliyokua nayo. usipende kuhukumu vitu usivovijua

Hizi ni moja ya njozi nzuri sana.

  1. Ujamaa uliachwa rasmi na CCM kwa kupitisha azimio la Zanzibar. Azimio la Arusha ni njozi kwa ulimwengu wa sasa.
  2. Ufisadi huimarika pale serikali inapoamua kuzima vyombo rasmi vya wananchi vya kuihoji na kuisimamia serikali.
  3. Elimu bure ni changa la macho. Fedha zote za halmashauri zimepelekwa serikali kuu, halafu hazitumwi za kuwezesha hata ukarabati wa vyoo.
  4. Kwenye kodi mpaka waziri wa fedha anasema kwenye hotuba yake kuwa kodi zimekuwa kandamizi kwa wafanyabiashara hivyo kuathiri ukuaji wa hali ya maisha ya watu.
  5. Kuhusu kiswahili hapo unapoteza muda wako kusifia mambo ya kijinga kabisa. EAC wote wapo kwenye kingereza hadi Rwanda kaamua kuhama kutoka kifaransa kwenda kingereza na siyo kiswahili. Kiswahili itabaki lugha ya mazungumzo tu na kufanya mambo yetu humuhumu. Naona hii hoja ya lugha umeiweka kiuchokozi zaidi, ili kupata reaction uliyoilenga.

All the best.

Hakuna uthbitisho wa ilo usemalo ila muda utaongea

Mada za hivi zinafaa huko kwenye jukwaa lenu jipya la tuzungumzeforum.com maana huko watu wanaosifia hata ujinga.

Ni hivi, Magufuli hafuati azimio la Arusha bali ana tabia zake za makuzi ambazo hazina utaratibu maalum. Kama kuna mambo yanakaribiana na azimio la Arusha sio lengo lake bali ni bahati mbaya. Halafu nikuambie kitu, kwa dunia ya sasa Azimio la Arusha ni mambo ya siasa za kujengana woga wawala hazina tija yoyote. Dunia ya sasa ni ya soko huria na bidhaa bora ndio zinazotamba. Katika ya sasa mtu kama Magufuli ni ngumu kufanikiwa kwani hajui lolote kwenye uchumi zaidi ya maamuzi ya mihemko.

Ndio maana unaona uchumi unazidi kudondoka na yeye kutegemea mikopo zaidi ambay nayo hana muda ataikosa. Hiyo miradi anayowekeza hela nyingi haijafanywa tathmini, bali anaifanya kwa kiburi cha madaraka na kusaka sifa binafsi. Hadi leo hajatoa ajira mpya zaidi ya lugha za kejeli kutokana na ulevi wa madaraka. Tulikuwa tunapiga kelele kuhusu usiri wa mikataba ya madini, sasa hivi yeye siri ni mpaka kwenye mapato kwa kuwa anajua mambo hayaendi vizuri. Simply anaiharibu nchi na namna pekee ni kuzuia nguvu yoyote ya kuhoji sera zake mbovu.

Mada za hivi zinafaa huko kwenye jukwaa lenu jipya la tuzungumzeforum.com maana huko watu wanaosifia hata ujinga.

Ni hivi, Magufuli hafuati azimio la Arusha bali ana tabia zake za makuzi ambazo hazina utaratibu maalum. Kama kuna mambo yanakaribiana na azimio la Arusha sio lengo lake bali ni bahati mbaya. Halafu nikuambie kitu, kwa dunia ya sasa Azimio la Arusha ni mambo ya siasa za kujengana woga wawala hazina tija yoyote. Dunia ya sasa ni ya soko huria na bidhaa bora ndio zinazotamba. Katika ya sasa mtu kama Magufuli ni ngumu kufanikiwa kwani hajui lolote kwenye uchumi zaidi ya maamuzi ya mihemko.

Ndio maana unaona uchumi unazidi kudondoka na yeye kutegemea mikopo zaidi ambay nayo hana muda ataikosa. Hiyo miradi anayowekeza hela nyingi haijafanywa tathmini, bali anaifanya kwa kiburi cha madaraka na kusaka sifa binafsi. Hadi leo hajatoa ajira mpya zaidi ya lugha za kejeli kutokana na ulevi wa madaraka. Tulikuwa tunapiga kelele kuhusu usiri wa mikataba ya madini, sasa hivi yeye siri ni mpaka kwenye mapato kwa kuwa anajua mambo hayaendi vizuri. Simply anaiharibu nchi na namna pekee ni kuzuia nguvu yoyote ya kuhoji sera zake mbovu.

Zidumu fikra za mwenyekiti

Sina hakika sana kama ile misingi ya lililokuwa Azimio la Arusha unaijua!

Magufuli anachokifanya kupambana na watu wema na wenye machungu na rasilimali za nchi hii kama akina Lissu ni roho mbaya yake ya kutaka kuabudiwa ambayo haiko kwenye Azimio LA Arusha

Magufuli hapambani na ufisadi, anapambana na wale wabaya wake walio na tuhuma mbalimbali za ufisadi na wengine anapambana nao kwa chuki zake binafsi tu lkn hawana tuhuma zozote za kijinai

Angekuwa anapambana na ufisadi kwa nia njema na taifa hili angeanza na aliyenunua kivuko kibovu kile cha Bagamoyo (MV Dar es salaam) kilichogharimu mabilioni ya walalahoi wa nchi hii ambacho hakikuwahi hata kwenda route moja tofouti na ile route ya uzinduzi aliyoifanya yeye mwenyewe Magufuli akiwa Waziri wa ujenzi wakati huo

Wako wapi waliotajwa kwenye report ya makinikia kama wasababisha hasara wa matrilioni ya makinikia serikali?

Wale viongozi wa serikali waliohusika na Escrow wako wapi maana tunaona wapokea hela tu wako korokoroni lakini walioruhusu mabilioni hayo yatoke wako uraiani wanakula mema ya nchi hii

Magufuli angekuwa anasimamia kwenye misingi ya azimio LA arusha asingekuwa ana roho mbaya kiasi cha kuleta ubaguzi kwa baadhi ya jamii na jamii nyingine kuiona kwake ni bora zaidi

Magufuli ni mvunja katiba na sheria za nchi, hivyo kumfananisha matendo yake na azimio LA Arusha ni kulitusi azimio hilo

Watu wanachukia double standards ambazo Mwalimu Nyerere hakua nazo angalau kwa waziwazi. Kama Mwalimu angekua ameendesha oparation ya wenye vyeti fake asingemkingia kifua yeyote tena waziwazi kama ilivyofanyika katika oparation hii ya sasa, na mfano wa mambo mengi sana ya hayo ndio yanafanya watu wasikubali ulinganifu wa awamu hizi mbili

Najua mnajua jinsi mambo yanavyoendeshwa kwa sasa… basi tu hamna namna… na mnapenda kupima watu imani na kusikilizia upepo…

Ila time will tell…

Cc: @Mahondaw

Drama tu si ametangaza anapewa mshahara wa mil 9 kwa mwezi.Kweli anaenzi azimio

hivi dunia ya leo unawezaje kumsifu mtu anaefuata azimio la Arusha??? ni siasa za hovyo kabisa zilizo itumbukiza nchi kwenye umasikini wa kutupwa na uongozi mbovu. NI AIBU MTU KUJISIFU KUA ANAISHI AZIMIO LA ARUSHA

Pale utekerezwaji wa Azimio la Arusha unapoladhimisha teknolojia ya mitandao ipewe masharti magumu ili kuzuia uozo uliojificha wa boss wako.

Daaah,umetufata mpaka huku!!!

Azimio la Arusha lilikuwa linahubiri Ujamaa.
Kuhubiri ujamaa karne hii ni kuonekana kituko.
Huwezi ukaendelea kwa sera za ujamaa kama huna maarifa yakutosha wala huzalishi Teknolojia yoyote.
Kwa Africa Ujamaa ni kugawana umaskini tu.

Tusidanganyane eti kurudisha Ujamaa ndio kutatufanya tuendelee , ndio kwanza tunarudi nyuma.
Ujamaa hautaki watu wawe matajiri natuona jiwe linavyowachukia matajiri, Ujamaa hautaki mawazo huru na tunaona jiwe linavyokazana kuzima wanaomkosoa.

KWA KIFUPI AZIMIO LA ARUSHA LINA SERA ZA KIMASKINI TU.

Vipi kuhusu ujamaa wa china na ulaya mashariki? Je umeleta umasikini kama unavyodai?