Jaribu kuangalia upepo usije ukadondosha shilingi chooni.

Ma dada ni kweli hakuna anaependa kuitwa maharage ya Mbeya maji mara moja. Lakini angalia upepo kwanza na majibu unayotoa.

Mkaka anakutokea unamwambia mimi nina mtu wangu, kumbe wala mtu huna, ulitegemea atafanya uchunguzi kwanza ndiyo agundue kuwa unamdanganya. Wengine hawapendi matatizo na watu wanaamua kutafuta aliye single anaendelea na safari.

Baada ya muda ameoa na imetokea mnaishi mtaa mmoja, tena wewe una grocery pale mtaani. Kumbe bado una fundo moyoni hata mkewe akija kununua mahitaji humchekei.

Wengine wanajibu mimi siko tayari kuwa na mpenzi sasa hivi. Mmh mwanaume akiacha kumtafuta baada ya mwezi anaanza kumtafuta kwa simu na kuuliizia habari zake kwa watu.

Msikilize jamaa atakavyopresent hoja zake. Kama huna jibu mwambie nipe muda. Kama unaamini Mungu, ukifika nyumbani liweke kwenye maombi Mungu atakuingoza. Kama una watu wa karibu unaowaamini unaweza kuomba ushauri.

Usikurupuke pia tunapenda kuona mnaiendeleza dunia.

Wengine wanasema wanakula bata/ujana kwanza.

Anataka aonje kila aina ya bamia na mihogo mtaani hadi mtaa wa pili.

Akishiba na kukinai huku ladha ishakatika kama jembe linavyoisha makali baada ya kulimiwa kwenye kila aina ardhi.

Wadada tambueni thamani yenu na fanyeni maamuzi sahihi, uong una pande mbili(hasi na chanya) kama ilivyo mambo mengine.

Wakati unausema huo uongo pima kwanza mizani ya matokeo yake ambayo ni hasi au chanya halafu ndio uuseme.

Pale unapostuka wale uliowaringia wana watoto chuo na secondary

Asante kwa kutukumbusha maa

Hapo unampigia mbuzi gitaa, huwa wagumu kuelewa hao

‘Kama unaamini Mungu, ukifika nyumbani liweke kwenye maombi Mungu atakuongoza’,hii ndio njia sahihi kabisa…

Naomba niwatakie Jumapili njema.
Kwa wale wa mrwngo wa huku, nawaomba tusiache kwenda kuabudu/kusali

Mada zako nzuri…zina ureality na maisha haya ya kitanzania

:p:p

Sidhani kama watakuelewa, ngoja tuone

Ujumbe mzuri sana…

dawa ya moto ni moto

Pia wajihadhari maana mwanamke kaumbiwa kutongozwa, wasije wakakubali kila anaeomba mechi, kwa kigezo asije poteza bahati.

Wadada mnaojikuta mkuje huku mpate somo…

wengi humu wako vzr, wasiojielew kbs wapo instagram n fb

:D:D:D:D:D:D

Hata humu wamo tena wengi tu

Mkuu umekitoa wapi hiki kicheko cha CHAMA?

Wasipoelewa na hapa hatuna kingine cha kuwasaidia.
Tatizo wadada wakiona kuna at least watu 4 wanamtongoza ndio nyodo huwa nyingiiiiii baadae yanakuwa yae ya Mchagua Nazi…

Emoji za vicheko humu ni adimu tunalazimika kutumia hicho cha chama mkuu