Mbuzi wa shughuli mathalani NDAFU hupitia pilikapilika nyingi sana mfano kutolewa mazingira yake aliyokuwa ameyazoea na kupelekwa asikokujua tena akiwa na kamba shingoni sasa akikumbuka Kule alikotoka yeye ndiye alikuwa mbabe,mtawala wa majike kadhaa anajikuta akihangaika kutaka kukimbia saa zote huku pia hofu ya kisu ikimzidishia wasiwasi…sasa yeye Hussein machozi anasema hana wasiwasi kwani yeye siyo mbuzi wa shughuli akimaanisha kuwa hamhofii mkewe kwenda kutafuta chakula iwe sokoni au kufanya biashara yeye atajipumzisha tu home hana wasiwasi na mkewe,anamwamini…