Dhambi iliyo mbaya kuliko zote

Nawasalimu wote kwa hisani ya majirani zetu Wakenya wenye uhuru wa kweli. Na kweli humweka mtu huru.
Kila mtu anajua kuwa kwa mila za Kiafrika hasa Tanzania ni jambo la aibu na fedheha baba mzazi kumwingilia binti yake wa kumzaa.
Katika dhambi isiyovumilika ni hiyo na huweza kupelekea hata binti aliyeingiliwa kujiua kukwepa fedheha atayoipata kwa jamii.

Tanzania ya leo imeanza kulaaniwa kwa matendo yasiyofaa kama haya ya kuwaingilia mabinti wa kuzaa wenyewe aidha kwa kuwalazimisha au kwa kuwarubuni vyote havikubaliki. Matukio haya yamekua yakitokea sana ktk jamii zetu na yamekua yakifumbiwa macho kwa kuhofia kubambikwa kesi na wahusika hasa wakiwa ni wakubwa kwa maana wenye vyeo vitukufu.

Nimalizie maoni yangu kwa kuwaasa wote waliofanya mchezo huu watubu haraka sana ili nchi yetu ianze kukua kiuchumi, kijamii, kisayansi na kitekinolojia.
Pia nawakemea wote wafanyao mchezo huo wakome mara moja, hii ni fedheha jamani hata Mungu hapendi uchafu huu.
Mbarikiwe sana kwa hisani ya majirani zetu. Ndimi mkimbizi mwenzenu.

:oops::oops: nanukuu “Matukio haya yamekua yakitokea sana ktk jamii zetu na zimekua zikifumbiwa macho kwa kuhofia kubambikwa kesi na wahusika hasa wakiwa ni wakubwa kwa maana wenye vyeo vitukufu”:rolleyes::rolleyes:

Haaaaaahaaaaaaaa

Tangu Babu Seya alivyoalikwa kunywa chai Ikulu mpaka leo hii mimi bado nashindwa kushangaa kabisa.

Nakwambia hii nchi inavyopelekwa ni Mungu mwenyewe ndo anajua mwisho wake.

Walaaniwe wote wafanyao hiyo dhambi!

So sad!

Wakibambwa wahasiwe.

Hivi ni kweli jiwe nalo liliwahifanyaga hivyo kwa yule bintiye mpaka akajiua?

Beautiful country…

I love my country, Tanzania

Amwingilie na yule kilaza wake J labda akili zinaweza kufanya kazi na kufaulu masomo yake

mmh! hii message mbona kama inataka kumlenga mtu fulani,okay by the way waliofanya ushetani huu watubu ili nchi yetu ikue kiuchumi. ova!

Hii message haimlengi mtu mmoja ila inawalenga wote wenye tabia hizo.

Inasikitisha sana…

Cc: @Mahondaw

Kama wapo wababa wa namna hii inabidi wanaume tuwatafute tuwasute. Heshima ya binti yangu inafanana sana na heshima ninayompa mama yangu mzazi. Ni karaha na inaleta ukakasi kusikia mambo haya ya kimapepo

Haya mambo yapo kwenye jamii na mbaya zaidi yanafanywa na watu ambao tungetegemea wawe mfano wa kuigwa, inasononesha sana.