Chakubanga huna ubavu wa kupambana na Zitto

SUNDAY, JULY 1, 2018
Zitto, Polepole wavutana mtandaoni kisa Mwigulu

Kwa ufupi
Ni baada ya Zitto kumpa pole Mwigulu na kueleza kuwa aliponzwa na msimamo wake kuhusu Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)

By Raymond Kaminyoge, Mwananchi [email protected]

Dar es Salaam. Mambo yamekuwa mambo mitandaoni. Ndivyo unavyoweza kusema kutokana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Humphrey Polepole na Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe kuvutana katika mtandao wa kijamii wa Twitter kuhusu mabadiliko madogo ya baraza la mawaziri.

Katika mabadiliko hayo yaliyofanywa na Rais John Magufuli, Mwigulu Nchemba ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ameachwa.

Zitto aliandika katika ukurasa wake, “ndugu yangu Mwigulu Nchemba karibu back bencha ufanye kazi ya wananchi. Tunajua msimamo wako kuhusu barua ya KKKT (Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania) umekuponza, ulikuwa na msimamo madhubuti na ulisimamia haki.”

Baada ya Zitto kuandika hayo, Polepole aliibuka na kumjibu, “mzee wa kurukia treni kwa mbele ushaanza, mbona unapenda ubashiri na vitendo vya kilozi. Rais hutenda impendezavyo kwa dhamana aliyopewa na Katiba.”

“Sisi tuliohudumu kwenye serikali na chama tunajua na kuheshimu, usijitatafutie huruma kwa mtu acha kupotosha hiyo si siasa safi.”

Katika mabadiliko hayo, nafasi ya Mwigulu imechukuliwa na Kangi Lugola ambaye awali alikuwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Chakubanga katika “ubora” wake!

Cha

Chaku na Nchemba.,…nani zaidi!!!

Ktk jamii zilizo staarabika Mwigulu alitakiwa kuwa gerezani kama mfungwa.

Tunapo elekea, hata hao anao wateuwa wataanza kugoma na kuzikataa nafasi hizi za kuteuliwa kwasababu hawana Imani na anae wateuwa, na anawafukuza kama mbwa… tehteehhh

Dhamana aliyopewa na katiba IPI? After all, “Katiba sio kipaumbele changu”… rejea maneno ya mkuu. Chakubanga huna hoja kabisa, sio lazima uandike kama huna cha kuandika!!

Mzee wa kwenda na moja kichwani.hivi kwani alijua hiyo moja hua wana kwenda nayo miguuni?.chakubanga

Kipaumbele chake ni udikteta, wizi, uongo, ufisadi na uuaji wa Watanzania wasio na hatia.

Chakubanga is really clueless and rudderless. Zitto amebainisha tu hisia zake. Chakubanga anarukia kumkataza kuwa hisia na kumkejeli! Hao ndio viongozi wetu! Ridiculous. No wonder Kinana ameamua kujiondokea.

Haaaahaaaaa. Huyu polepole sijui ana nini kichwani. Sidhani kama mzima.

Mwigulu ana roho mbaya sana ya ukatili, ila roho yake ipo kwenye chama zaidi kuliko serikalini.

Waziri wa mambo ya ndani inabidi uwe roho ya ukatili kuliko ngosha mwenyewe, maana hiyo ndio wizara inayompa kiburi na jeuri zote.

Chakubanga alishabakiza fuvu tu, ubongo alikabidhi kwa jiwe amtunzie

Mkuu tukifikia huko itakuwa bomba sana. Unadhani huyu Mwigulu anaweza kuamua kupambana na dikteta chini kwa chini akishirikiana na MACCM wengine ili wampige chini 2020? Au atahofia?

Singida United chalk, haitaweza kuendeshwa kwa account y mbunge ya jimbo

Chakubanga amebakishiwa akili za kwendea chooni tu.

Chakubanga kweli ubora wake na ngarungaru

Hivi kuna mtu ashawahi kukataa uteuzi?

Mambo mengine yaacheni kama yalivyo…

Cc: @Mahondaw

Haaaa haaa who is Chakubanga

Ni kizee fulani hivi kiropokaji hapo lumumba, ndiyo kilikuwa kidalali cha kununua wapinzani uchwara, kilipiga hela nyingi sana kwenye hiyo project kimestukiwa ndiyo maana manunuzi yamekoma.