Ajali hiyo imetokea leo Juni 25 saa 10 alfajiri katika eneo la Dundani wilayani Mkuranga Mkoani Pwani.
Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga Dk Stephen Mwandambo amethibitisha vifo hivyo, amesema maiti za watu 14 zimepokelewa na kuhifadhiwa katika chumba cha maiti hospitalini hapo.
“Ni kweli hili tukio limetokea alfajiri, tumepokea miili 14 na majeruhi wanne,” amesema Dk Mwandambo.
Kwa barabara hii ya kilwa hususani kuanzia kongowe serikali lazima ichukue hatua hasa kwa haya malori ya michanga kwani daaaa!!!wanaendesha kama ndio watumiaji pekee wa barabara!!hususani usiku kwani wengi wao wanakesha na ndio maana hata huyo aliyesababisha ajari alikuwa amesinzia!!!na wengi wanaoyandesha wanakuwa ni makondakta tu na sio dreva!!!yeye anataka umpishe hata akiwa anakuja upande wako wewe ndio uingie polini kumkwepa!!
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amepokea kwa mshtuko na masikitiko taarifa ya vifo vya watu 14 waliopoteza maisha baada ya basi dogo walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori la kubebea mchanga katika eneo la Dundani Wilaya ya Mkuranga Mkoani Pwani.
Ajali hii imetokea tarehe 25 Juni, 2018 saa 10:40 Alfajiri wakati basi dogo lililowabeba wanafamilia, ndugu na jamaa waliokuwa wakielekea Msata kuhudhuria sherehe za kumaliza mafunzo ya kijeshi kwa mtoto wao, kugongana uso kwa uso na lori lililokuwa linatoka Dar es Salaam kwenda Dundani kuchukua mchanga. “Naomba unifikishie pole nyingi kwa wanafamilia wote waliopatwa na msiba, waambie naungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majozi ya kuondokewa na wapendwa wao, na sote tuwaombee Marehemu wote wapumzishwe mahali pema peponi” amesema Mhe. Rais Magufuli katika salamu zake za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo.
Mhe. Rais Magufuli pia amewaombea majeruhi 4 wa ajali hiyo wapone haraka ili waweze kuungana na familia zao na kuendelea na majukumu yao ya kila siku.
Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
25 Juni, 2018
Kama Dereva wa Lori usiku mzima badala ya Kulala ili mwili upumzike vizuri Yeye anakuwa juu ya Kiuno cha ’ Malaya ’ huku akikatiwa Viuno vya kila aina unategemea ’ akidamka ’ asubuhi kuanza majukumu yake hatosinzia na kupelekea kusababisha hizo ajali?
Mkuu Eli kwanza natoa pole kwa wote waliopoteza ndugu zao na pole nyingi kwa Majeruhi. Na Mungu awapumzishe panapostahili marehemu wote. Hila mkuu tafadhari taharifa za huyo chogolee jiwe tunaomba huku zisiandikwe kabisa maana jamaa hana imani na mitandao na ndo kasababisha tupo ukimbizini kwa sasa. Huku habari zije lakini sio kuhusu huyo bwege bana.
Yaani wanafungia mtandao wetu halafu bado mnaleta taarifa zao huku. Hizi mngewaachia Uhuru, Jamvi la habari, Tanzanite, Daily news na Tazama bila kusahau tbc