A bit of Poetry

[CENTER]
Lesson Learned

So, sato niliamka bila form

Indoors, nikasema leo sidai kuroam

Kutulia tu kiasi, nikaskia phone

Nganya ya me inanicall

Kakanishow, “home kuna party”

“Pilau kwa wingi na machapati”

Heee, kusikia ati party? Machapati?

Mimi huyo, trao, viatu na shati

So, kwa matt nikaelekea kwao kejani

Kakanipick tukaingia ndani

Masalamu, nikaketi, yangu nikaletewa sahani

Kwenya ngohe, chapati, thufu na biryani

Nikajilea vizuri bila kujali

Kwa meza wakaleta wali

Bila kusleki, nikamega kaugali

Nganya ya me nikiikemba tu kwa umbali

So, nilibonya vizuri nikashiba

Tumbo furi furi bila shida

Story zikaanza, watu kujuana

Hapo ndo nikakumbuka

Heee, na si nimemanga sana

Kwanzia supu na mamutura za jana

Supper, kathembe na nyama

Breko, hivo hivo kama jana

Alafu sahi, lawama

Hapo ndo tumbo ilianza kuleta balaa

Nikajua leo nayo nimepatikana

Hapa lazima niondokee hizi jamaa

Hapa itabidii nimeunda sana

Teke, nikarauka, na kusaka mama

Nikamshow naunda, tumbo imeleta noma

Kakacheka na kunishow niache ufala

Niaje na manga alafu nadai kuhepa

Enyewe nikaona ata mimi nimeingiza za ovyo

Kakanisho, maybe nitafeel poa nikienda choo

Nakapenda, so nikagree, hio loo kakanishow

Manze hapo ndo saa maneno ilianza kuflow

Choo ilikuwa just next to sito

Nikaingia teke, nilikuwa nimekazwa vi soo

Mlango nikafunga na kuketi, ready to go

Maneno, wacha zianze kuflow

Si mchezo, nilikuwa nimemanga sana

Mizinga tu nilikuwa naangusha ka osama

Each drop, kwa moyo nikifeel, hapo sawa

Vile tu shughuli nimemada

Trao kuvaa na kupull kamba

Blunder

Tank empty, hakuna waba

Hee, sema mwanaume kutense

Stranded, already choo nimemess

Nikashindwa saa hapa what next

Kutoa simu, nganya kutext

Niaje babe, hii choo yenu haina maji

Na already nishamaliza kazi

Hakureply, nikajua hapa nayo nitatii

Vile nilikuwa narusha mizuka na bidii

What such a pity

So, kwa choo nikakaa for about an hour

Mawazo huku inanigonga sawa sawa

Aii, arufu ikazidi, nikasema hapana

Hii ni mchezo, wacha niache ufala

So, pole pole door nikafungua

Nakukemba rada kama kuna mtu najua

Hakuna raiya, wazi, mimi huyo nikajitoa

Nikeanda kusaka mama pahali alikua

Kwa harakati zangu, nganya nikaipata

But it was too late

Buda yake alikuwa asha fyetu

Alienda choo, akapata mamess tu

Hee, ka ni wewe ungefanya nini

Ju mi naye nilijifanya si mimi

Ikabidii ni watoi wamebeba musalaba

Teke teke wakaambiwa wasake waba

Hahaha, choo ilisafishwa mara moja

Despite that, sherehe ikaendelea bila hoja

Nganya yangu huku ilishinda ikinicheka

But, do I care

Lesson Learned

Ukienda party

Mizigo yako

Peleka kwako

Ama utatii

[/CENTER]

3 Likes

Too long, weka summary!

ho ho hoo NV keti paree

@rasGavos una talanta boss.

1 Like

Thanks