Pamoja na Dr Stephen Ulimboka kuponea tundu la sindano kwa kipigo cha wasiojulikana hata baada ya gazeti pendwa Mwanahalisi kumtambua na kumwandika Ramadhani Ighondu mwajiriwa wa usalama wa taifa kuhusika.
Pamoja na Azori Gwanda kuchukuliwa na watu waliotambulika kutoka serikalini na kupotezwa na mkewe kuendelea kupewa matumaini kuwa yupo katika mikono ya sheria atapatikana
Pamoja na Ben Saanane kupotea na kila dalili na ushahidi hata wa polisi kukiri amechukuliwa na usalama wa taifa na simu yake kuendelea kupatikana katika maeneo ya ofisi za PSU kijitonyama
Pamoja na Roma mkatoliki kutekwa na kuteswa kwa muda na mkuu wa mkoa wa Dsm kuahidi angepatikana baada ya siku tatu na kweli akapatikana
Pamoja na ushambuliaji wa Lissu kutokea na ushahidi wa namba za magari na watu waliokuwa wanamfuatilia kutolewa hadharani na kukosekana hata nzi katika mikono ya vyombo vya dola vya nchi hii
Pamoja na matukio mbalimbali ya utekaji na kuzamisha watu kwenye maji mengi ambao hakuna maelezo muafaka hadi leo hii
Juzi tena huko songea yametukia mambo ya ajabu ya utekaji na kunyanganya form za uongozi madiwani wa Chadema chini ya mtutu wa bunduki!
Juzi jamaa mmoja wa tarime Peter Zacharia kidogo atufumbulie fumbo lakini dola imekataa.
SERIKALI IMEKANA WAZI WAZI KUWA HAIHUSIKI!!
Tufanyeje?
Serikali imekana wazi wazi na tumepigwa marufuku kuihusisha na mambo hayo.
Tumebaki peke yetu!!
Mawazo/mapendekezo yangu
Haya ni majambazi ni lazima wananchi tuungane kupambana nayo.
Tutawalinda viongozi wetu na wale wanaotafuta uongozi kupitia vyama vyote.
Tukiwatia nguvuni ni kipigo cha mbwa koko ikiwezekana kutia kiberiti. Serikali itatupengeza sana kwa kuisadia kuondoa hii HEADACHE!!