UMUHIMU WA SWALA KATIKA UISLAMU

Dini ya kiislamu ambayo Mwenyezi Mungu ameitukuza na kuridhia nayo, na ameweka malipo makubwa kwa vile vinavyotamani nafsi na uislamu umejengwa na misingi na hatosalimika anaekeuka misingi hayo na adhabu iumizayo, na atakae fuata misingi hayo atapata utukufu na heshima hapa duniani na kesho akhera, na miongoni mwa misingi hayo ni swala, swala ambao ni msingi wa dini na nguzo ya pili baada ya kutamka shahada mbili, na swala ni fadhila kubwa ambapo Mtume wa Mwenyezi Mungu (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) amesema: [ Swala ni bora, na atakae weza kuzidisha basi na azidishe].

Swala ni nguzo ya pili katika uislamu. Imepokewa na Anas akisema Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) : [Nimependekezwa na wanawake mafuta mazuri na nikajaaliwa kuwa swala ndio kitulizo cha macho yangu]. Na ni ibada ya kwanza aliyofaradhisha Mwenyezi Mungu, na mwanzo atakayohisabiwa mwanadamu, na ndio wasia wa mwisho ambao Mtume (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam) ameusia umma wake akisema: [ Swala, swala na watumwa wenu]. Na ndio mwanzo itakayopotea na ikipotea imepotea dini.

Na kuonyesha umuhimu wa swala kufaradhishwa katika mbingu ya saba, na ndio inaowekwa mafungamano kati ya mja na mola wake, na inakataza maovu. Amesema Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Taala):

قال تعالى) : إِنَّ الصَّلَاةَ تَنْهَى عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنْكَرِ( [العنكبوت: 45] {{Hakika Swala humzuilia huyo mwenye kusali na mambo machafu na maovu}}