umuhimu wa lugha ni communication

Tafadhalini waTanzania nawaomba mtambue kuwa hata sisi waKenya tunafahamu Kiswahili. Acheni kulalamika kuwa Kiswahili chetu ni kibovu. Kiswahili is a compulsory subject for all Kenyans from primary school up to form 4 level (12 years of learning Kiswahili) but tunapenda kutumia sheng coz hiyo ndio “Ukenya” wetu. hata waNigeria na waJamaica wako na Kiingereza chao but zote ni informal English na bado inawasaidia kuuza mziki na inatambulika dunia mzima…hata Kingereza cha Marekani, Uingereza, Australia zinatofautina kabisa ilhali asili yao ni moja. Tambueni hilo

Ni kweli kuwa sio wakenua wote ambao hawawezi kuandika na kuzungumza kiswahili fasaha hasa cha lahaja ya kiunguja ambayo bisa shaka ndiyo iliyosanifishwa ya kuwa ndo kiswahili fasaha kuzungumzwa. Watu wa pwani ya kenya (mombasa, malindi, lamu nk) huwa wanazungumza kiswahili safi sana na huenda usijue kama ni mtu kutoka viunga vya kenya.

Ila inabidi mkubali tu uzaifu wenu hususan wengi mtokao kenya bara japokuwa mmekua mkifunzwa somo la kiswahili hadi form 4 ila mmeshindwa kabisa kukizungumza kwa fasaha na kwaharaka. Askari wenu wakigundua ya kuwa waliemtia mbaroni ni mtanzania basi hatupewi nafasi ya kujitetea kwa kuwa wanajua wazi lugha ni shida kwao.

Kusema ya kwamba ninyi mnazungumza sheng nfo maana kiswahili sanifu hamkiwezi hio sio sababu kwani hata sisi wenyewe watz tuna swanglish na simo nyingi sana, ila ikifika pahala panapotakiwa kuzungunza sarufi sanifu huwa tunatiririka kama kawaida.

Tumeshatambua Mkuu, ongeeni tu hyo sheng hakuna shida. ila hata sisi wabongo kiswazi chetu cha mtaa hamtakiweza, tuelewane tu hvi hivi ila hyo lugha ya Malkia muda mwingine ni changamoto

siwezi kukupinga ila matumizi ya sheng sio kwa sababu hatuwezi kutumia Kiswahili sanifu. ni njia ya kujitambulisha. utakuta sheng ya Dandora ikiwa tofauti na sheng ya Kibra. wote ni wakaazi wa Nairobi ila wanatumia sheng tofauti ili kujitambulisha kwa mtaa wao na kujitofautisha na mitaa mingine

Sina shaka nikibaini kwamba, mleta uzi ni mjaluo… tehteehhh

Kuna wenzio huwa wanakiponda Kiswahili na kutukuza Uzungu…