Tenzi za rohon

Bwana Mungu, nashangaa kabisa, nikitazama kama vilivyo,
nyota, ngurumo, vitu vingi vyote, viumbwavyo kwa uwezo wako.

Roho yangu na ikuimbie, jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie, jinsi wewe ulivyo mkuu.

Nikitembea pote duniani, ndege huimba nawasikia,
milima hupendeza macho sana, upepo nao nafurahia.

Nikikumbuka kama wewe Mungu, ulivyompleleka mwanao,
afe azichukue dhambi zetu, kuyatambua ni vigumu mno.

Yesu mwokozi utakaporudi, kunichukua kwenda mbinguni,
nitashukuru na kwimba milele, wote wajue jinsi ulivyo.

Neno

Roho yangu na ikuimbie, jinsi wewe ulivyo mkuu,
Roho yangu na ikuimbie, jinsi wewe ulivyo mkuu…

Cha kutumaini sina, ila damu yake Bwana
Sina wema wa kutosha, dhambi zangu kuziosha

Kwake Yesu nasimama, ndiye Mwamba ni salama
Ndiye Mwamba ni salama, ndiye Mwamba ni salama

Damu yake na sadaka, nategemea daima
Yote chini yakiisha, Mwokozi atanitosha.

Kwake Yesu nasimama, ndiye Mwamba ni salama
Ndiye Mwamba ni salama, ndiye Mwamba ni salama

Njia yangu iwe ndefu, Yeye hunipa wokovu
Mawimbi yakinipiga, nguvu zake ndiyo nanga

Kwake Yesu nasimama, ndiye Mwamba ni salama
Ndiye Mwamba ni salama, ndiye Mwamba ni salama

Nikiitwa hukumuni, rohoni nina amani
Nikivikwa haki yake, sina hofu mbele yake

Kwake Yesu nasimama, ndiye Mwamba ni salama
Ndiye Mwamba ni salama, ndiye Mwamba ni salama

Ubarikiwe

Yesu ndiye kiongozi wangu…kumfuata yeye ni furaha…ajuaye kuongoza vyema…
anilinda nisione shida…analeta raho moyoni…

Mwimbieni Bwana hii…

Naupenda ndio maana nimeuweka hapa

Tenzi za Rohoni… zina ushuhuda mkubwa sana…

Nyimbo za tenzi nzuri sana haswa ukiziimba kutoka ktk vilindi vya nafsi na roho yako hujisikia kuhuishwa

Twende kwa Yesu mimi nawe,
Njia atwonya tuijue
Imo Chuoni; na Mwenyewe,
Hapa asema, Njoo!

Na furaha tutaiona,
Mioyo ikitakata sana,
Kwako, Mwokozi, kuonona,
Na milele kukaa.

“Wana na waje,” atwambia.
Furahini mkisikia;
Ndiye mfalme wetu pia,
Na tumtii, Njoo.

Wangojeani? Leo yupo;
Sikiza sana asemapo;
Huruma zake zikwitapo,
Ewe kijana, Njoo.

Amen

LIKO LANGO MOJA WAZI

1.Liko lango moja wazi, Ni
lango la mbinguni; Na wote
waingiao Watapata nafasi.

%Lango ndiye Yesu Bwana
Wote waingie kwake,
Lango! Lango La Mbinguni
ni wazi.

2.Yesu ndiye lango hili, Hata
sasa ni wazi, Kwa wakubwa
na wadogo, Tajiri na maskini.

3.Hili ni lango la raha, Ni lango
la rehema; Kila mtu apitaye
Hana majonzi tena.

4.Tukipita lango hili Tutatua
mizigo, Tuliochukua kwanza,
Tutavikwa uzima.

5.Hima ndugu tuingie Lango
halijafungwa, Likifungwa mara
moja Halitafunguliwa.

AKIFA YESU NIKAFA NAYE

1.Akifa Yesu nikafa naye
Uzima upya huishi naye;
Humtazama mpaka nje:
Nyakati zote ni wake yeye.

%Nyakati zote nimo
pendoni, Nyakati zote ni
uzimani, Humtazama hata
atokee, Nyakati zote mimi
ni wake.

  1. Vita sipigi visivyo haki, Na
    Bwana wangu hapiganiki;
    Beramu yake haitwaliki, Napo
    po pote hila sitaki.

  2. Sina mashaka, akawa
    mbali; Mizigo yote aihimili;
    Ananituliza Imanweli, Nyakati
    zote mimi husali.

  3. Sina huzuni na mimi sidhii;
    Simwagi chozi, wala siguni;
    Sikuti afa, ila kitini Daima
    hunifikiri mimi.

  4. Kila unyonge huusikia; Kila
    ugonjwa kwake hupoa; Yesu
    ni mwenye kuniokoa Nyakati
    zote hunijalia.

Mungu ni pendo apenda watu,
Mungu ni pendo anipenda

Sikilizeni furaha yangu,
Mungu ni pendo, anipenda

Nilipotea katika dhambi,
nikawa mtumwa wa shetani

Akaja Yesu kuniokoa,
yeye kanipa kuwa huru

Sababu hii namtumikia,
namsifu yeye siku zote.

N

natafuta hiyo audio ya huu wimbo OG

Unaweza pata google,u tube hata playstore zitakuwepo application zenye audio

Kote sijafanikiwa nimeutafuta sana

Good Sunday

@Ntolilo nimekupenda