Taarifa iliyotolewa na TCRA ni ya uongo na upotoshaji mkubwa

Nimeisoma taarifa iliyotolewa kwa Umma na TCRA tarehe 16/6/2018 kwa kile ilichokiita upotoshwaji unaofanywa mitandaoni kuhusiana na kufungwa kwa mitandao ya kijamii na Blogs nchini Tanzania

Katika barua hiyo ambayo inakanusha kuwa mamlaka hiyo ya Mawasiliano hawana mpango wa kufuatilia wale wanaotumia mitandao ya kijamii kama vile Facebook, Instagram na tweeter

Barua ile ni ya upotoshaji mkubwa kwa kuwa tunajua kuwa watawala wa Tanzania wanafanya kila juhudi kuona kuwa hakuna mtanzaniia yeyote anayeweza kuikosoa serikali hiyo aidha ni kupitia kwenye vyombo vya TV na radio na Magazeti hapa nchini

Ni ukweli usiopingika kuwa hapa Tanzania vyombo vya habari vyote vya Umma na vya binafsi vimedhibitiwa vilivyo na mamlaka za utawala nchini Tanzania

Na vyombo vilivyothubutu kuikosoa serikali hii ya awamu ya 5 viliishia kupigwa faini au kufungiwa kabisa

Kwa hiyo watanzania kwa mamilioni wamekosoa mamlaka nchini ya kuingilia Uhuru wa TV na radio na magazeti ya Tanzania kutokana na vyombo hivyo kuwa na kazi moja tu ya kuusifu utawala wa Magufuli na serikali yake kuwa unatupeleka kwenye kula asali na maziwa!

Vile vyombo vilivyojaribu kuikosoa serikali hii ya awamu ya 5 walikiona cha moto!

Nitataja baadhi ya vyombo vya habari vilivyoonja joto ya jiwe, Mwanahalisi na Mawio ni mfano wa dhahiri ya namna serikali hii ya kidhalimu ilichowafanyia kwa kuwafungia maisha yasichapishe makala zake tena!

Kwa hiyo watanzania wakabaki na option moja pekee ya kupata habari zao “balanced stories” na si pengine Bali ni Jamii Forum, ambako nako makucha ya TCRA yamefika na kuwafungia, lengo ni kuwataka wamiliki wake wawajibike kwa mabandiko ya watumiaji wake!

Kwa hiyo hao TCRA wanafanya ghiliba kubwa chini ya utawala huu wa Magufuli wemye lengo la kuminya Uhuru wa vyombo vya habari ambao ni kinyume kabisa cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2005, ibara ya 18(1) inayotamka wazi kuwa " Kila raia wa Tanzania atakuwa huru kutoa mawazo yake kwenye chombo chochote na Uhuru huo haupaswi kuingiliwa na chombo chochote" mwisho wa kunukuu

Mungu ibariki Tanzania

anhaaa baada ya kusoma taarifa ya tcra sasa nenda kasome na sheria ilofanyiwa marekebisho ndo uje na kitu kinachoeleweka.

Mkuu itapendeza sana kama itatuwekea hapa hiyo taarifa ya Jana ya tcra

Sijaelewa
Umekuja kukanusha au nini?

Nilivyomwelewa ni kwamba anakanusha kanusho la TCRA!

Akiwa kama nani yeye?

That’s right

Kama raia wa Tanzani na kwa mujibu wa Ibara ya 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano Tanzania anayo haki ya kutoa mawazo yake!

tcra wasijisumbue kabisa kukanusha maana nia yao ovu inafahamika kwahiyo wananchi wanafanya kujiongeza tu

Eewa kuwa tuna haki ya kujadili mambo yanayohusu maslahi yetu wewe kada wa Lumumba!

Bora umempasulia ukweli huyo kada wa Lumumba asiyejua hata haki zake za kikatiba za Raia wa Tanzania

Unaipinga barua kwa barua ipi??

Barua ya posa ama ya msiba!!

Nyir

Nyie watu wa Lumumba vishtobe kweli kweli,We unahoji kama nani?

We mchawi umekuja na huku…kazi kweli kweli

Pengine sijasoma kwa uzuri kilichoandikwa,

Halafu kwanini mnaniita Lumumba?

Lumumba kwangu ni tusi, mnitake radhi aisee.

Mkumbuke huku sio kwetu tupo ukimbizini, yale mambo ya kucharurana tuyaache. Wenzio walidhani wewe ni Lumumba ila mimi nilielewa kwamba hukusoma ukaelewa alichoandika @Wonder Boy .

Nimekusoma mkuu.

Muwasamehe misukule wa lumumba, hawana akili bali wanaishi kwa kutumia “fikra za mwenyekiti”.
TCRA you are on the wrong side of history, you will be remembered as one of the instruments that Jiwe used to oppress the people. Curse you mathafantas

Hapa Ukimbizini pako poa