serikali ya JPM yakwama

ni wazi sio siri tena serikali ya awamu ya tano,imekwama kiuchumi,kitendo cha magu kutembeza bakuli kwa wa machinga kwa kisingizio cha vitambulisho ni wazi kabisa mbio za sakafuni zimeanza kuishia ukingoni,haya ni madhara ya one man show,nchi inakufa kiuchumi,wamachinga ni kundi la watu linalotafuta tonge ili siku iende,ni vijana waliochoka kimaisha ,wasijue kesho yao,leo unakwenda kuwakaba kwa kuwatoza 20000/=.eti wakilipa hawatasumbuliwa.
serikali ya awamu ya tano imekosa ubunifu,ubunifu ni sifuri,ni serikali iliyojikita kwenye kutoa vitisho na ubabe mwingi,kimsingi uchumi wa tanzania ni wa udongo unahitaji kumbelezwa wao ndio kwanza wanakuja na maji ili kuutest,angalia mafao ya wastaafu 25% nimambo yasiyoweza kuingia kwa mtu mwenye akili hai,ni wazi nchi inaelekea shimoni,miaka inaenda 4 sasa hakuna ajira kwa vijana,vijana hawajui kesho yao umri unaenda.ni wazi serikali ya awamu ya tano inapenda sifa isiyostahili na inafanya maendeleo kwa kutafuta sifa,ukiangalia swala la ununuzi wa ndege za ATCL ni TAMAAA tu ya mtawala,hakukuwa na sababuyoyote ya ununuzi wandege kwa fedha za walala hoi,wakati mashirika ya ndege binafsi na ya gharama nafuu yapo,ujenzi wa standard gauge railway pia ni TAMAAA ya maendeleo makubwa na sifa ukilinganisha na hali ya uchumi ya wananchi wetu,leo ukiangalia hali za wananchi kimasha zinasikitisha,watu wanashindwa kununua dawa ,elimu imeshuka inaelekea shimoni
jakaya kikwete hakushindwa kufanya haya YOTE,ANGEWEZA TENA KUPITA HATA YA SASA,jk asingeshindwa kutulea mandege ya kila aina hata
standard gauge railway angejenga hadi vijijini,lakini busara na hekima vilimtawala jk,hakuwa na tamaa ya NAENDELEO MAKUBWA,ndio maana wastaafu walistafu na faraja,vijana walipata ajira mpaka wakazikimbia,hakuwatoza kodi wamachinga,nchi ilikuwa niya neema

Na bado huu ndiyo mwanzo wa mwisho wa CCM

Miye hili lijamaa lisingekuwa jizi ningelitetea kwa uzalendo wa kutetea waafrika lakini vile vile ni jizi pamoja na mavibaka bashite!! I hate them. Ningeangalia labda linakosa uzoefu wa uongozi lakini shida ni JIZI

Mmmh,tuombeane

Mdogo mdogo tutafika…

Cc: @Mahondaw