Rais Magufuli umepotosha hakuna waraka wa kanisa unaotolewa na wanasiasa

Nimemsikia Rais Magufuli akisema alipokuwa akitembelea ujenzi wa msikiti mkubwa wa BAKWATA hapo majuzi kuwa viongozi wa dini wasiruhusu wanasiasa kuwa ndiyo wasemaji wao

Naamini alilipiga hilo "dongo’ kuongelea ule waraka uliojipatia umaarufu mkubwa wa kanisa la KKKT uliotolewa wakati wa sikukuu ya Pasaka ya mwaka huu

Nimekuwa nikijiuliza hivi ule waraka ni kweli uliandaliwa na wanasiasa na baadaye ukasomwa na maaskofu??

Jibu nililolipata ni HAPANA kubwa sana kwa kuwa ninaamini kuwa waraka ule uliaandaliwa na maaskofu wa kanisa hilo kubwa hapa nchini la KKKT wakiongozwa na roho mtakatifu wa Mungu na waliweka na saini zao pale chini

Nimekuwa nikijiuliza je ni kitu gani kilichomfanya Rais ahusishe ule waraka na wanasiasa??

Jibu nililolipata ni kuwa Rais alipata kiwewe baada ya waraka ule kutoka, kwa kuwa yeye amezoea kusifiwa na kupambwa tu kuwa anawafanyia mema watanzania

Ule waraka ulikuja tofauti kwa kuwa ulielezea mapungufu mengi ya serikali ya awamu ya 5 ambayo serikali hii inapaswa iyafanyie kazi iwapo itataka nchi yetu iendelee kuwa na umoja wa kitaifa ambao tumeendelea kuwa nao tokea tupate Uhuru.

Umoja huo kwa Mara ya kwanza tumeanza kuona unatikiswa chini ya utawala huu wa Magufuli

Kwa hiyo kutokana na tamko lile la Rais ambslo naamini hakulitoa kwa Bahati mbaya ninadiriki kusema kuwa Rais amepotoka kwa kusema kuwa makanisa yana wasemaji wao ambao ni wanasiasa, ninachoamini Mimi ni kuwa makanisa yana wasemaji wake wenyewe ambao ni maaskofu wakiongozwa na roho mtakatifu wa Mungu na sivyo anavyotaka kutupotosha yeye Magufuli

Mungu ibariki Tanzania

Na huyo Magufuli alitoa kauli hiyo kwenye shughuli iliyohusisha BAKWATA kwa kuwa anajua viongozi wake amewaweka mfukoni

Ni kwa nini kauli hiyo hakuitoa kwenye shughuli ya kanisa, hususani KKKT ambao ndiyo waliouandika waraka ule??

Yapo maswali mengi yanayokosa majibu

Huyo jamaaa kwa sasa anahaha tuu. Fulll upuuzi.

Aisee

Ni kama amedata hivi.

Ipo siku atajikuta pekee yake.

Yaani kabisa ni kama anaingia uchizi vile!

waraka unamkuna naona hivi karibuni ataenda kuswali masjid, maana ndo chaka lake kwa sasa

Anapenda kuona anasifiwa muda wote hataki kukosolewa.Ukimkosoa tu anahisi unatumiwa na baadhi ya wanasiasa

Kazi sana ukipenda kusifiwa kubali na kukosolewa…

Jiwe akikosolewa anawashwawashwa. Alafu tulianzaje kuchagua mtu anaitwa POMBE??:frowning:

Nafikiri hapa aliwalenga kina Mbatia na wenzie baada ya kuwataka KKKT wasijibu chochote kuhusu ike barua

Karibu sana dadake huku ukimbizini

Jamaa muoga mno hana confidence kabisa utafikiri ni mjinga fulani hivi asiyejielewa hata kidogo

kwanini anaogopa wanasiasa kiasi hiki

Mambo na taarifa kama hizi za uchambuzi ndiyo yanayoitesa JamiiForums Tanzania…

Hawataki kusikia taarifa kama hizi… wanataka mawazo yako yashindwe na yalegee…

Cc: @Mahondaw

Mimi mwenyewe nilishangaa sana,kwanini alitoa kauli ile…kwa kweli inabidi hawa viongozi wetu wakae chini waangalie ni wapi wamekosea…tunarudi nyuma sana kiuchumi,kidiplomasia,kimuunganiko kama taifa.

Jamaa kwa uongo hana mpinzani.wewe mtu anasea eti aliongea na marehemu kombani akiwa I.c.u

Yaani siku ile nilijua jamaa ni tatizo. Anaamini wanasiasa wana akili sana kuliko maaskofu kiasi kwamba maaskofu hawaoni tatizo lolote bali wanasubiri wanasiasa wawaelekeze cha kuongea! !

Kwenye sikukuu ya Iddi ndio nikaona mashehe Bakwata wakitema yale mashairi waliyomezeshwa na mkulu. Wao kazi yao ikawa kushambulia viongozi wa kikristo waliotoa nyaraka. Ni bahati taasisi ya kiisilamu ya kina shehe Ponda wametoa waraka stahiki kwa serekali hiyo jana.

Awamu hii tutashuhudia kila aina ya unafiki toka kwa viongozi mbalimbali wa dini na siasa

Kiv