Rais Magufuli hafai kuongoza nchi yenye mfumo wa vyama vingi

Nianze bandiko langu kwa kunukuu Katiba ya Jamhuri ya Tanzania, ya mwaka 1977, iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2005, ibara ya 3 ambayo inasema hivi " Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania itakuwa ni nchi ya kidemokrasia, yenye kufuata mfumo wa vyama vingi" mwisho wa kunukuu

Nimeanza bandiko langu kwa kunukuu kifungu hicho cha Katiba, ili tuone kwa vitendo na hulka yake huyu Rais Magufuli, kama kweli anafaa kuongoza nchi ya mfumo wa vyama vingi

Mara tu alipoingia madarakani, alionyesha dalili za kutotaka kukosolewa kwa kuondoa Bunge Live…

Akaja tena kupiga marufuku mikutano yote ya vyama vya upinzani hadi mwaka 2020…

Ndipo Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akatoa onyo mwaka Jana, kuwa huyu mtu akishamaliza kuumaliza upinzani atakuja kwenu CCM na kuhakikisha kuwa hakuna kauli yoyote ya kumpinga itakayotoka ndani ya CCM

Wakati ule alipoongea Tundu Lissu, wanaccm waliona kama ni “stories” tu za Tundu Lissu, lakini kutokana na kauli aliyoitoa Rais Magufuli kwenye kuapishwa kwa Waziri mpya wa mambo ya ndani, Kangi Lugola, ndipo alipothibitisha usemi wa Tundu Lissu!

Alinukuliwa akitoa onyo Kali sana kwa wabunge wa CCM wa mikoa ya Kusini, akina Hawa Ghasia na Nape Nnauye kuwa kama wabunge hao wangeendelea kuipinga serikali yake kupora pesa za wakulima wa korosho asilimia 65 za “export levy” angeanza kwanza kuwapiga shangazi zao hao wabunge wa CCM waliokuwa mstari wa mbele katika kuipinga hiyo Sera mpya ya CCM

Vile vile tumeshuhudia viongozi wakuu wa Chadema wakihangaishwa na kesi zisizokuwa na kichwa wala miguu, zenye Lengo la kutaka kuwafunga

Hivi hao viongozi wa Chadema wamefanya kosa gani iwapo nchi yetu ina mfumo wa vyama vingi na wajibu mkubwa wa viongozi wa upinzani ni kuikosoa serikali ili irudi kwenye mstari kwa manufaa ya nchi

Hebu jaribu kuimagine ile kampuni ya utafiti ya Twaweza, kila mwaka wanatoa matokeo ya tafiti zao…

Mwaka juzi walitoa tafiti yao kuwa Rais Magufuli anakubalika na watanzania asilimia 96

Mwaka Jana wakatoa matokeo ya utafiti wao kuwa Rais Magufuli anakubalika kwa asimia 71

Wakati wote huo hatujaona kampuni hiyo ikipata misukosuko, lakini mwaka huu walipotoa matokeo ya utafiti wao kuwa Rais Magufuli ameporomoka sana umaarufu wake hadi kufikia asilimia 55, ndipo serikali imewalima barua ijieleze ilipata wapi kibali cha kufanya utafiti huo na isopotoa maelezo ndani ya siku 7 “kibano” kitawakumba!

Nimekuwa nikijiuliza mbona siku za nyuma wamekuwa wakitoa ripoti zao, lakini vyombo vya dola vimekuwa haviwagusi??

Au ni kwa sababu wamekuwa wakimpamba Rais Magufuli kuwa umaarufu wake umekuwa ukiendelea kupaa??

Lakini wakati kampuni hiyo imetoa tafiti yake kuwa umaarufu wa Magufuli umeshuka, ndiyo “nongwa” imeanza!

Jamaa anapenda sana sifa
Nalog off

Hatuna rais kwa sasa.

Amevuruga kila kitu

Anafanya uteuzi siyo kwa kuzingatia sifa, Bali kwa wale watakaokuwa wa kupokea maagizo toka juu…

Hata kusema hafai kuwa rais kwenye mfumo wa vyama vingi bado umempa sifa asiyostahili (maana itaeleweka kuwa anafaa kuwa rais kwenye mfumo wa chama kimoja). Ukweli ni kuwa Magufuli hafai kuwa Rais katika mazingira yeyote yale

You are absolutely correct by 100%

Kuna kiongozi na mtawala…

Magufuli hana hata sifa ya kuitwa mtawala. Mtawala (anaweza asiwe democratic ila anajua na ana uhakika wa kile anachotaka kifanyike). Mahathir Mohammed wa Malaysia ni mtawala (alipochukua mamlaka Malaysia ilikuwa maskini kuliko Tanzania yetu, hakuwafanya waliokuwa matajiri wawe maskini ila alijitahidi maskini wawe matajiri). Aliemuita Megafooly hakukosea hata chembe

Huyu Jiwe hafit kokote…

Mtu ambaye anatamani wale waliokuwa wakiishi kama malaika, waishi kama mashetani, huyo siyo kiongozi wala mtawala!

Umenena vyema mkuu.

Kingunge(R.I.P) aliwahi kusema anafaa kuwa mnyamparaa tu

Shida kubwa sana

Anafaa kuongoza Taasisi lakini si Nchi tena kubwa kama Tanzania, Wizara ilimfaa sana

napita kimywa kimywa…

Hata hivyo vyama vingi ni jina tu kwa sasa, ila kiukweli nchi inaongozwa na chama kimoja

Failure

Ngoja tuone…

Cc: @Mahondaw