Rais Magufuli amethibitisha kuwa Bunge la Tanzania ameligeuza kuwa rubber stamp yake!

Kwa wale tuliomsikiliza akilihutubia Taifa wakati wa kuapishwa kwa Waziri mpya wa mambo ya ndani, Kangi Lugola, aliyechukua nafasi ya mtangulizi wake, Mwigulu Nchemba, ambaye ametimuliwa uwaziri, atakubaliana nami kuwa, katika hotuba yake hiyo, Rais Magufuli amethibitisha kuwa Bunge siyo tena mhimili unaojitegemea, ambao wajibu wake mkubwa ni kuikosoa serikali kwa lengo la kutenda haki kwa wananchi wake, na badala yake amethibitisha kuwa Bunge hilo ameliweka mfukoni na analiagiza kutoka Ikulu kwa remote contro kwa yale anayotaka yeye yafanyike!

Siyo vyema kurejea kila kitu alichokisema, lakini nitanukuu baadhi ya mambo muhimu aliyoyaongea ambayo kwa kweli kwa maoni yangu hayapaswi kuongelewa na Mkuu wa nchi

Baadhi ya maneno aliyoyatamka ni kama yafuatayo:-

  1. Nilisikia kwenye kikao kilichoisha cha Bunge baadhi ya wabunge wa CCM wakitishia kutoipigia kura ya Ndiyo bajeti hiyo, kwa kile walichokiita kuibiwa pesa za wakulima wao wa korosho na kutishia kuandamana iwapo pesa hizo hazitoridi. Waandamane tu na wakione cha moto na Mimi ningeanza kuwachapa shangazi zao ndiyo wajue kuwa Mimi siyo mtu wa mchezo mchezo!

  2. Nilimuuliza Waziri Mkuu kuna wabunge wangapi wa CCM wa mikoa ya Kusini, akanijibu ni 17, nikamwambia Waziri Mkuu kuwa waache waondoke na watuachie CCM yetu na hatutayumba kwa kuwa bado koram ya kuongoza Taifa hili itakuwa upande wetu

  3. Nilimwagiza Katibu Mkuu wa CCM, Bashiru achukue mahudhurio (roll call) na nikaagiza kuwa wabunge wote wa CCM ambao hawatakuwepo wakati wa kuipitisha bajeti hiyo awalime barua za warning!

Nimekuwa nikijiuliza hivi hao wabunge wa CCM wa serikali ya awamu ya 5 hawana tena uwezo wa kuikosoa serikali yao, kwa mujibu wa Katiba ya nchi??

Kama wanao kwa kuwa wao ndiyo wawakilishi wa waliowachagua na wamewatuma wawasemee hayo waliyoyasema, nimekuwa nikijiuliza hivi kuna sababu zipi za msingi za kuwatisha wabunge hao/kiasi hicho??

Nimekuwa pia nikijiuliza, hivi akina Nape Nnauye na Hawa Ghasia ni wabunge wa kuchaguliwa na wananchi wa mikoa ya Kusini au ni wabunge wa kuteuliwa na Rais??

Ukipata majibu ya maswali hayo ndipo hapo utakapothibitisha kuwa Bunge limepokwa madaraka yake ya kuwa ni Mhimili unaojitegemea na hivi sasa umewekwa mfukoni mwa Jiwe na analicontrol kwa remote control akiwa pale Magogoni!

Ee Mwenyezi Mungu tufanyie wepesi wa kutuondolea huyu mtu ambaye hataki kabisa kabisa hata kule kupewa constructive criticism kwa lengo la kuijenga nchi yetu

Asante Mungu unazidi kutuangazia mwanga wa kuona ni aina gani ya serikali ipo madarakani, hatuhitaji tena Tundu Lissu aje atupe somo kila mwenye akili ameelewa.

Mwacheni Mwenyekiti awaadabishe wabunge wa chama chake. Hali hii itaendelea hadi pale watakapojitambua na kupigania suala la Katiba kumtambua mgombea binafsi…

Time will tell…

Cc: @Mahondaw

Sio Bure ,lipo jambo karibuni, Ibilisi wake anazidi MPA kiburi na roho ngumu ili yatimie maandiko yaliyo tamkwa na kina Lisu na wenye hekima wengine.

Cha kujiuliza ni ikiwa bunge ni genge la kupitisha atakacho jiwe,sasa kwanini wanaruhusu mijadara?.

huyu maji marefu kafanya kosa kubwa sana kufariki bila kutuagulia huyu mtu, haya sasa hv ndo nini?

Ni ajabu na kweli

wanasema limewekwa mfukoni…! hawafurukuti wanaogopa posho kukatwa!

Angefanya mazingaombwe yake, ili jiwe aone mauza uza ili arudi kwenye mstari

Hatuna bunge kwa sasa. Tuna upuuzi tu pale.

Hatuna Bunge tuna kundi la walanguzi na wachumia tumbo

Alichokifanya ni kujibu swali la Pasco Mayalla, bunge lingesubili kidogo jibu wangepata bila ya kumuita Pasco, japo jibu walikuwa nalo tayari.

[FONT=tahoma]Hakika haina maana ya kuwa nalo kama wabunge wanapigwa mkwara kuwa wasipopitisha bajeti bunge litavunjwa na hakuna mwenye uhakika wa kurudi tuna bahati mbaya sana kuwa na viongozi wasioheshimu katiba wala mihimili mingine. Majaji wastaafu waheshimiwa Jaji Ramadhani na Jaji Samata walijaribu kuwa wawazi kwa namba moja juu ya misingi ya haki na kufata sheria wakatoa mifano ya uvunjifu wa haki wa matamko ya wakuu wa mikoa na wilaya waliongea mambo mazito sana ni juu ya namba moja kuyazingatia au kuyapuuzia maana wao waliitwa kutoa yao ya moyoni na wameyasema.[/FONT]

kazi yangu ilikuwa ni kupitia kila mchango…

…nadhani rais anajua mipaka na wajibu wake vizuri…

Yupi huyu jiwe au