NETFLIX kwenye TV

Kama kichwa kinavyojieleza naombeni mwenye kujua ama kufahamu hiyo NETFLIX kwenye TV inatumikaje na je unaweza kuitumia kwa internet peke yake au kunanjia nyingine zaid ya internet inaweza kutumika na kuonesha vile uvitakavyo?

Natanguliza shukrani wakuu

ngoja waje wataalamu

sijawahi itumia ila najua kuitumia lazima ulipie. Wanatengeneza series na Movies na kuziuza kwenye site yao. Kutumia lazima uwe na smart TV, uwe ujijisubscribe huko kwa kulipia na bando, Hakuna njia nyingine Lakini Movies walizotengeneza au series zao unaweza kuzipirate torrent kama movies zingine tu.

nashukuru mkuu, nimepata mwanga

  1. ni lazima uwe na internet kuitumia
  2. inapatikana kwenye vifaa mbalimbali kama vya android, ios na windows.

kama una smart tv kuna uwezekano mkubwa inakubali netflix ama tayari imeshawekwa. bei yake ni dola 10 kwa mwezi na unaweza ukashare na wenzako ila mwisho ni vifaa viwili kwa mpigo.

kama huna smart tv unaweza ukanunua tv box na kuiweka smart tv kwenye tv yako ya kawaida.

vitu vyote vya netflix yaani hizo movies na series vinapatikana online kirahisi kama alivyosema mdau hapo juu ama ukatumia app kama terrarium kuziona ila kama una uwezo nakushauri unga netflix au jichange na mwenzako muwe munashare gharama sababu itakuondolea headache ya vitu kama
-matangazo huko utakapozipata hivyo vitu hasa kwenye tv yanakera.
-server ambazo zipo slow zitakazofanya movie igande gande ama kama unadownload ichukue muda.

Hivi vitu kwa speed ya internet ya Tz ni kujidanganya tu

hapana netflix wana hadi sd ambayo unastream na internet ya ovyo kabisa chini ya 250KBps kama utakuwa huna internet nzuri.

issue ni kifurishi cha unlimited ili kui enjoy ndio tabu kupata unless unaishi mjini city centre kabisa ambapo kuna broadband nzuri au unaishi miji ya mikoani ambapo kuna smart ndio utafaidi hii netflix.