Ndizi na nyama.

MAHITAJI
1.Ndizi mbichi
2.Nyama robo
3.Nyanya kubwa(Tungule) 4
4.Nazi moja kubwa
5.Ndimu 1
6.Karoti 1
7.Pilipili Hoho(Pilipili boga)1
8.Kitunguu maji kikubwa 1
9.Kitunguu thomu punje 3
10.Nyanya ya Paket vijiko vya chakula 2
11.Royco(Sio lazima)
12.Tangawizi na kitunguu thomu ilotwangwa kijiko cha chakula 1

MAANDALIZI
1.Osha viungo vyako vyote vinavyotakiwa kuoshwa
2.Katakata Nyanya,Kitunguu maji,thomu,Pilipili hoho weka kwenye blenda na uvisage vyote
3.Kuna nazi yako na ichuje
4.Weka tui zito na jepesi mbalimbali

JINSI YA KUPIKA
1.Chemsha nyama uloiweka tangawizi kitunguu thomu na chumvi mpaka iwive
2.Chemsha ndizi weka pembeni
3.Weka nyanya ulizozisaga kwenye nyama yako acha ziive
5.Weka nyanya ya paketi na Royco
6.Weka chumvi na ndimu kama imepungua ongeza chumvi kidogo
7.Weka tui jepesi kwenye ndizi na chumvi acha zichemke kwa dakika 3 usikoroge
8.Kisha weka tui zito acha lichemke kwa dakika 2
9.Weka mchuzi wako wa nyama acha kwa dakika 2 epua
10.Acha zipoe kidogo pakua kwenye sahani tayari kwa kula

NB: 1.Hakikisha mchuzi unakua mzito mzito na mdogo
2. Pika ndizi zako kwa moto wa wastani ili zisigande kwenye sufuria
3.Epuka kukoroga wakati wa kuzipika ndizi zako
4.Kama utataka kukoroga chukua tambara safi shika sufuria yako itikise au chukua banio la ugali bana kwenye sufuria na uitikise

Dadeki…ila nyama ni kidogo sana…Mimi napenda nyama nyingi aisee…halafu na parachichi.

We n mchaga?? Kwenye parachichi hapo umenikumbusha nilikua namix na makande enzi naishi moshi n vitam balaa

Hoyeeee!

Hahahhaa

Na upishi wa makande utufundishe [COLOR=rgb(150, 150, 150)]

Ngoja nikae kitako nitaandika

Shabash! unitag nisichelewe