Namna ya kumuosha maiti

  1. Maiti awekwe juu ya kitanda cha kuoshewa, kisha afinikwe uchi wake, kisha avuliwe nguo zake, afichwe na macho ya watu ndani ya chumba au mfano wake.
  2. Inapendekezwa kwa muoshaji atatie kitambaa mkononi mwake wakati wa kuosha.
  3. Muoshaji atakiinuwa kichwa cha maiti akaribie kumkalisha, kisha apitishe mkono wake kwenye tumbo lake na alikamue, kisha aisafishe tupu yake ya mbele na ya nyuma kwa kuosha najisi yoyote iliyopo.
  4. Muoshaji atanuilia kuosha na atapiga bismillahi.
  5. Muoshaji atamtawadhisha maiti kama udhu wa Swala, isipokuwa katika kusukutua na kupaliza puani, huwa inatosha kumpukusa kinywa na pua.
  6. Atakiosha kichwa cha maiti na ndevu zake kwa maji ya mkunazi au sabuni au kinginecho.
  7. Ataosha sehemu ya kulia kisha sehemu ya kushoto, kisha atakamilisha sehemu ya mwili iliyosalia.
  8. Inapendekezwa atie kafuri katika osho la mwisho.
  9. Atampangusa maiti.
  10. Amuondolee maiti vitu vinavyotakikana kuviondoa kama kucha, nywele za kinena (nywele za sehemu ya siri) na makapwa.
  11. Atazisuka mkili nywele za mwanamke aziweke nyuma yake
    https://www.kenyatalk.com/index.php?forums/jukwaa-la-elimu.50/post-thread