Kosa kubwa alilolifanya Melo ni Kutii Sheria

Kwenda kujipeleka TCRA na kujisajili hili kosa kubwa sana na amebugi(hapa kaingia kwenye mtego)
Umaarufu wa JF hautakuwa kama ule wa zamani.

Wengi tulitarajia angehamishia Ofisi nje na JF ingekuwa ina operate kama ilivyo Facebook na mitandao mingine.

Jamaa kashaingia kwenye mtego.

kwani kaenda kujisajili tcra?

Ngoja niweke akiba ya maneno

Me too!

Naikumbuka sana ile hadithi ya ‘Heri mimi sijasema’…

Mmmh mkuu kwanza hizo pesa za kujisajili ulichangia hata senti? Max akienda jela kwa kosa la JF je utaweza msaidia kumlipia gharama za wakili?

Lawama nyingine ni uzwazwa,mwenyewe max na wenzake wanaelewa wakifanyacho so utake usitake JF sio mali ya watanzania bali ya Jamiimedia.

Gharama za kuhamia nje sio pesa ndogo,all in all masimango kwa max hayasaidii,kama mlipiga kelele mswada kandamizi usisainiwe na ukasainiwa na hapa sheria kandamizi ya wadau wa korosho nayo imepita. Jua kwamba vita si ndogo kama mnavyofikiria

Wewe umewahi lala hata selo siku moja…!?

Una hata kablogu!??

Ungesoma kwa utulivu nilichoandika hasa hapo nilipoweka mabano pengine ungenielewa, sijamuhukumu melo ila nimeangalia mustakabali wa wote.(wao na wateja)

Samahani kama nimesomeka Kinegative.

Ndio ila hawataki kusaini.

Hapo wanamkwepa.

Nimesoma pote na ndo maana nimekujibu kirefu jinsi nilivyoelewa bandiko lako. Unaposema angehamishia nje ina maana na yeye angehamia huko pia na familia yake,hapo hapo anabeba na akina invisible, paw na kadhalika na familia zao,kwa biashara ipi kwa mfano labda kama wangerudi kwa kutaka kila mwanachama atoe ada ya kuchangia JF kwa miezi,mwezi au mwaka.

msemo jamaa kabugi hii ni hukumu tosha

Wewe Ndio umebugi unataka KIKI kwa MELO na JF. Jarbu kukadilia tu garama za kampuni uko nje unakotaka ww waende kufanyia kazi.
Wakisema hata members wa JF tuwachangie bado atuna uwezo wa kulipia kuingia JF hata kwa wiki tu.

Ndio maana nakupenda…

subira ni mwl mzuri saana.mwishowe kila kitu kitajulikana.tuwe na subira tuu wapendwa katika fikra huru.

Waaaoww

Unavyorespond vizuri kuhusu hili swala la JF,…hopefully unajua mengi behind

niliandika uzi kua kuna watu wanamlaumu Melo ila kuna waliopinga, haya sasa mfn hai huu hapa. Muda ni mwl mzuri sana, hv unapajua selo? Ushawah kukutana na figisu za Walumumba?, jukumu gani mfn leo Melo akikuomb ukamuwakilishe pale central ndan ya chemba ya mahakama dhidi wa mawakili na waendesha mashtaka wa lumumba kuitetea Jf utakubali na utaweza? . M nakuambia kama hujawah hata simamia kesi ya wizi wa kuku ukienda mahakaman ukakutana na figisu za wanalumba, utapigwa swali moja tu, utajibu yote mwenyewe mpk ambayo ulipaswa ukajib mbinguni. Ukitoka hapo unatangaza dau kwa wanaotaka kuinunua Jf mwenyewee, achana na kaz ya kupangua yale mwaswali pale kati wewe utataja mpk michepuko yako na watoto wa nje kwa jaji. Lets shut up our mouth and tune our typing finger…

Duuu, kwamba anajibu maswali aliyotakiwa ayajibu mbinguni, kisha ataje michepuko yake yote na watoto wao, watu mna maneno sijui mnatatoleaga wapi

Naona nimeeleweka vibaya kumradhi wana JF.

So ww uko kwa maslahi ya akina nani humu hasa?. Kama uko kwa maslahi na umetumwa na mafisisemu, go back home soon. Na nini kimekuleta huku wakati kule chama chenyu kimefunfia uhuru wa kujieleza?

sijakuelew hata