Hivi kulikuwa na ulazima wa kutumia risasi za moto kuzuia maandamano ya wanaChadema February 16?

Tumemsikia Kamanda wa kanda maalum ya Dar, Lazaro Mambo sasa, akitueleza kuwa wale waliiokuwa wakituhumiwa na mauaji ya mwanafunzi, Akwilina, aliyeuawa kwa kupigwa risasi akiwa ndani ya daladala, wameachiwa huru

Lakini Mimi sitajikita zaidi kwenye huo uamuzi aliofanya Kamanda Mambosasa, bali nitajikita zaidi kuangalia kama uamuzi wa kupiga risasi za moto moja kwa moja ulikuwa sahihi

Ninavyojua Mimi kabla ya operesheni yoyote ya kuzima maandamano, kuna taratibu ni lazima zifuatwe

Taratibu zenyewe ni hizi zifuatazo:-

Kwanza kabisa Mkuu wa kikosi kile cha kuzima maandamano hayo ni lazima awatangazie waandamanaji hao (huku akiwa anapeperusha bendera nyekundu) kuwa hayo ni maandamano haramu, kwa maana hiyo wayavunje

Analazimika Mkuu huyo wa kikosi, kurudia tangazo lake hilo zaidi ya Mara 3

Akiona bado waandamanaji hawataki kuitii amri yake, atayaagiza magari ya washawasha ambayo amekuja nayo kwanza kumwaga maji ya washawasha.

Akiona bado waandamanaji hao hawataki kutii amri yake, atalazimika kuamrisha hao askari kupiga risasi za Plastic

Hatua ya mwisho kabisa na baada ya kuona waandamanaji wanajibu mapigo kwa kikosi hicho na hivyo kuhatarisha amani, ndipo anapoweza kuamrisha hao askari wapige risasi za moto, tena siyo kwa nia ya kuuwa, Bali kupiga miguuni kwa lengo la kidhoofisha waandamanaji hao

Swali langu la msingi hapa ni je hatua zote hizo zilichukuliwa, kabla Mkuu huyo wa kikosi hicho cha kuzima maandamano yale kuamrisha aakari wake wapige risasi za moto??

Naungana na BAVICHA kutoa wito kwa Rais Magufuli aunde Tume ya kijaji ili iweze kuchunguza tukio hilo la kusikitisha sana lililosababisha kifo cha Mpendwa wetu, mwanafunzi wa NIT, Akwilina Akwiline

Hmm! Hii ndiyo nchi ya vi-wonder…

Jibu ni ndiyo kwa sababu nia ilikuwa kuua wala si kuzuia maandamano. Ila wakumbuke kila auaye kwa upanga naye atakufa kwa upanga, hata ipite miaka mingapi mauaji haya lazima yatakuja kuhojiwa, jela hazikujengewa wapinzani tu hata watawala kuna siku wataingia huko, Nawaz Sharif leo hii yuko wapi.

Ni jambo la kushangaza kusikia kuwa yule Polisi aliyefyatua risasi iliyonwua Akwilina ameachiwa huru!

Badala yake nasikia hilo zigo la mauaji ya Akwilina, huu utawala dhalimu unataka kiwabebesha viongozi wakuu wa Chadema!

Hakika ile kitu ya I WISH I COULD BE IGP ndiyo imeanza rasmi!

Jiwe alisema wazi wazi mchana kuwa “Fanyeni lolote nitawalida”, akiwaambia askari wake, polisi na sasa wanafanya kweli. Amemlinda ameonekana hana hatia!
hata miaka 1000, mauaji haya yatakuja kuhojiwa na tume huru na Jiwe atawekewa MSALABA WA MAUAJI KAMA HITLER AND HIS ACCOMPLICE BASHITE, MNYETI, GAMBA, MAMBOSASA, SIRRO … na wengine et al

Ulazima upo pale endapo waandamaji siyo chama tawala…

Cc: @Mahondaw

Alikuwa anatafutwa Mbowe maana Jiwe alishasema kuwa piiga mchungaji kondoo watawanyike!

Duh…

Hivi mtu waweza kuwa na roho mbaya kiasi hicho??

Mambo ya ajabu saaana.

HUYO NDIYE JIWE

hili jiwe sio litanzania ni linyarwandwa,na litatumaliza kwelikweli

Tena hakuwa police wa kawaida, inasemekana alikuwa ni mwanajeshi aliyevalishwa magadwa ya police kwa only one mission ya kumua mbowe

Haya yote uliyoyaandika ww ni ya muhimu sana kukumbushana ndani ya jeshi lile la kipolice. Ila cha ajabu wahusika hawajui kitu, wanafanya kazi kwa mizuka sana, hakuna cha mkubwa wao ama mdogo yaani wote km majuha vile. Wanajaribu kushindana na raia ambao hawana silaha aisee

Wao huwa wanatekeleza maagizo toka juu

Inasikitisha Sana’a

Alidhamiria kumuua Tundu Lissu, akamiminia risasi zaidi ya 30, lakini Mungu akakataa, Tundu Lissu anaendelea kudunda hadi Leo…

Amedhamiria kumuua Mbowe, lakini Mungu amemnusuru…

Hivi huyo jamaa, bado hajiulizi tu, iweje anapanga “mission” yake ya kuwamaliza viongozi wa Chadema, lakini Mungu si Athumani, wanaendelea kusurvive??

Kesi imegeuzwa wanasema viongozi wa chadema walikuwa na bastola mmoja wao ndio alipiga

Yetu macho

Imenenwa kuwa mwisho wa ubaya aibu!

Mkuu huo ndo msingi wa drama za police maana wanayo yafanya yana baraka zote kutoka kwa mzilankende.

Mambosasa hata haionei aibu familia yake.ni huyuhuyu alie twambia kua ni risasi ya police ndo ilikata kona na kuua.

Leo tena bila hata haya anasema eti viongozi wa cdm ndo walio kua na siraha.

Alitakiwa kwanza kuitisha press kukana yale maelezo yake ya mwanzo,kisha ndo aje na hizo helaya.

Kwa ujinga huu nani wa kuniaminisha kua jeshi la police ni kwa maslahi ya raia?.

Poleni familia ya mambo sasa.