Hadithi kali sana

HADITHI YA MTOTO NA MBWA MWITU
Mtoto mmoja, akiwa anarudi peke yake kutoka machungani wakati wa jioni, alipita katikati ya kichaka ambako alikutana na Mbwa mwitu. Kumbe yule Mbwa mwitu alikuwa na njaa na alijua kuwa mtoto kama yule angetosha kabisa kwa chakula cha jioni kwake na kwa familia yake ya watoto wanne kule pangoni. Alianza kumnyemelea akimmezea mate kwa uchu.
Yule mtoto aliogopa sana, mwili mzima ulitetema, ingawa alijitia ujasiri na hakutaka kufa kikondoo. Alifahamu ya kuwa hawezi kupambana naye kwa mabavu akamshinda, wala asingeliweza kushindana naye kwa mbio akamzidi.
Hivyo alipoona kwamba hakuwa na namna ya kujiepusha na hatari ile, alimgeukia Mbwa mwitu na kumwambia kwa unyenyekevu: “Najua, ee rafiki yangu Mbwa mwitu, ya kwamba u na njaa na mimi ni windo lako, na kwa kuwa sina uwezo wowote wa kujiokoa dhidi yako, basi kabla ya kuniua nakuomba unisaidie kitu kimoja tu. Nacho ni uniimbie wimbo mmoja niupendao ili nicheze kwa mara ya mwisho, kisha nikimaliza uniue na kunila.”
Mbwa mwitu aliangua kicheko kusikia ombi la mtoto ambaye kwake alikuwa tayari ni marehemu mtarajiwa. Baadaye alikubali, akachukua filimbi na kuanza kumpigia wimbo.
Wakati mtoto anacheza huku akiwa amejawa na hofu, Mbwa wa nyumbani kwake walisikia sauti ile, wakakimbilia pale kabla ya ule wimbo kwisha na kuanza kumtimua yule Mbwa mwitu.
Mbwa mwitu alimgeukia mtoto akasema, “Hii ni halali yangu; kwani mimi ambaye wasifu wangu ni muuaji na mla nyama, sikupaswa kugeuka mpiga filimbi ili kukidhi matakwa yako wewe.”

Kiswahili kitukuzwe…

Eka happy ending ghaseer

Tuelezee maudhui na maana fiche iliyoko ndani ya hii hadithi

From the mbwa mwitu

Strike while the iron is hot
Don’t count your chickens before they are hatched

From the kid

Ukishikwa shikamana
Papo kwa papo kamba hukata jiwe