Changu wa kukaanga

Mahitaji
Changu wazima au vipande
Limao
Chumvi
Pilipili
Mafuta

Jinsi ya kutengeneza
Osha samaki, toa matumbo na uwachanje chale
Twanga pilipili na chumvi kwenye kinu, ukipata paste iweke kwenye bakuli uikamulie limao
Paka paste ya chumvi, limao na pilipili kwenye samakii
Acha amarinate ikiwezekekana weka kwenye chujio la nazi chini weka sufuria ya kukinga maji.
Unaweza kuwaweka kwenye ungo ukaanika darini kama hakuna kunguru, mimi huwa ninaweka kwenye fridge kwa masaa 12.
Kukaanga, acha mafuta yapate moto, usipende kupika na moto mkali, kama ni jiko la umeme namba 4 inafaa

Samaki wa kukaanga kwa ugali, au wali maharage raha sana.

usione kimya, nakufuatilia sana kila cku kuna mtu nataka apate somo kwa ajili ya utengenezaji wa bites mbali mbali kuna fursa nimeona. Kuna ambazo ashajifunza kutoka humu tayar. asante na ubarikiwe

usione kimya, nakufuatilia sana kila cku kuna mtu nataka apate somo kwa ajili ya utengenezaji wa bites mbali mbali kuna fursa nimeona. Kuna ambazo ashajifunza kutoka humu tayar. asante na ubarikiwe

Shukrani, unataka nilete na bagia?

haswaaaaaa umejuaje? Na ubuyu wa zanzibar kama una ujuz nao

Yummy

Kumbe changu samaki, nilifikiri mtu