Kwa jinsi nilivyoona Belgium wanavyosakata kabumbu huko kwenye Ardhi ya Nchi ya Putin alikoweka Daktari wetu Mabilioni yakeya pesa almaarufu kama Mabilioni ya Urusi, ni dhahiri kabisa Belgium wanauwezo mkubwa wa kufika mbali na hata fainali au kutwaa ubingwa wa Kombe la Dunia.
Kwa sasa hatua ya mtoano ya 16 bora Belgium atakutana na Japan, na nina imani atashinda na kuelekea robo fainali, Brazil katika hii hatua atakutana na Mexico, Mexico ilionesha makucha yake tangu mwanzo ilipoilaza mabingwa wa tetezi-Germany bao 1 kwa nunge, wakati huo Brazil walilazimisha drawl ya na Uswizi ya kufungana bao 1 kwa 1. Katika mechi zilizofuata, Brazil ilishinda lakini sio kwa kiwango cha kuvutia sana ikizingatiwa wakati ilipokutana na Croatia ilishinda kwenye dakika za nyongeza baada ya kushindwa kufunga bao hata moja kwenye dakika 90.
Belgium imeonesha soka la nguvu lenye ustadi wa hali ya juu na kushinda mechi zake zote 3 kwenye hatua ya makundi.
Endapo Brazil atashinda kwenye hatua ya 16 bora ambapo atacheza na Mexico, Jee wakija kukutana na Belgium kwenye hatua ya Robo fainali ni ipi itagaragazwa…
Wadau wa mpira karibuni tutiririke kabisa juu ya tathmini kuhusu mwenendo wa hii michuano hasa hizi timu nilizozitaja hapa
Sorry mkuu, niliteleza kidogo kwenye vifupi vya Croatia (CRO) na Costa Rica (CRC) ndio nikataja Croatia,
Iilikutana na Costa Rica iliposhinda kwenye dakika za nyongeza