Kwa ufupi mazungumzo bado yanaendelea, wanaendelea kukubaliana namna bora zaidi ACACIA mshirika wa BARRICK ataendelea na uzalishaji wenye tija pande zote.Hawajaweka ukomo mazungumzo yatakwisha lini.Na makubaliano ya mwisho lazima yapate baraka Bodi ya wadhamini BARRICK.Habari njema maisha wataendelea chini ya ACACIA, zile tetesi Wachina kununua bado ni porojo.Zaidi pakua adobe press DOC.BARRICK
Tunasubiri Trilon 430 alizo sema bwana mkubwa na Parama Gamba Gumu
Walewale aliowaita wezi sasa hivi anakaa na kujadiliana nao.
JPM angekuwa amepata exposure japo kidogo tu, nina uhakika wala asingejiingiza kwenye usanii anaoufanya dhidi ya hawa Acacia / Barrick ambao ni “watoto wa mujini” kikwelikweli.
nao wamegundua jamaa yupo shallow sana kwenye reasoning - wanamchezea shere kadiri watakavyo.
Tushayazoea hayo
Hmm!.. :oops::oops::oops:
Vipi kuhusu kile kishika uchumba nacho bado kipo kwenye majadiliano.
Tumejngea reli ya kwenda Uganda mkuu
Serikali ingekuwa imefikia pazuri ingetoa taarifa haraka sana…kama kipindi like…ila nyie…Mungu anawaona
na wanavyo penda mapicha picha kama wasanii
Hili hautasikia mkuu akiimba nalo…atakaa kimya kama kwma wwmeiba Mawe ya kujengea vile…
Kumbe bado mazungumzo yanaendelea…
kwa hiyo ile kauli ya Waziri Profesa Kabudi kwamba mambo yanakwenda vizuri na hivi karibuni tutalipwa fedha, yalikuwa ni feki. Maana kama haijajulikana lini watafikia muafaka, na kwamba hata wakifikia muafaka na Barrick, itabidi hayo yote yathibitishwe na ACCACIA, sioni mwisho mzuri wa hili jambo. na hasa ukiangalia website ya ACCACIA wanalalamikia ripoti zote mbili za kamati zile zilizoundwa na JPM, halafu wanalipaje hizo fedha? tutasubiri sana
Nasikia kule kwenye ukuta wametokomea na madini kama upepo
Mtakaonichukia shauri zenu sipendi ’ Unafiki ’ ila niseme tu ’ tusidanganyane ’ hapa na kufanyana Wajinga kama siyo Wapumbavu hakuna ambacho Tanzania tutakipata katika hayo mazungumzo na kwa maoni yangu tu tukubali kwamba ’ tumeshaliwa ’ na tuanze nao tu upya kwa mustakabali mzima wa Sekta yenyewe na faida za baadae kwa Tanzania kama nchi na Watanzania pia.
Watu wa CCM na Waziri husika Profesa Kabudi tuache kulitumia hili kama ’ mtaji ’ wa Kisiasa na kutafuta ’ Sifa ’ kwa Watanzania kwani kwa ninavyowajua Wazungu na jinsi huo ’ Mtandao ’ wao wa ’ upigaji ’ ulivyokuwepo ambapo siyo Siri kuna ’ Wapigaji ’ wengine walikuwepo na baadhi yao pengine wapo hata katika Serikali ya sasa ni ngumu kufikia muafaka wake.
Tusipoteze muda na tusichoshane tukubali tu kuwa ’ tumeliwa ’ na sasa ’ tujizatiti ’ tu kwa baadae. Ahsanteni.
Hayo Mazungumzo ni sawa tu na yale ya kijiwe cha kawaha
Na pesa za korosho za wananchi wa kusini waambie wazipeleke…
hat ile ya mwanzo hawajalipa coz sijaona sherehe za kuipokea! jiwe hawez akapokea kimyakimya lzm angekikisha tu.
Jiwe mshamba sana .alichokoza mambo akaharibu kila kitu.sasa anapiga kimya na pesa hana kila Sikh kudanganya kwamba tunaenda right direction pesa ya korosho kala kashindwa kurudisha
chakubanga alisemaga tunalipwa yote trillion 430 ,wewe unaturudisha nyuma tena?