[FONT=courier new]Afrika itaendelea tu kama Siku moja wataamka, kuona umuhimu wa Rais Paul Kagame ’ Mwanamume wa Shoka na Shujaa wa Uchumi na Maendeleo ’ na kumruhusu awe Rais wa Bara la Afrika kwa miaka 10 tu ambapo ninaamini kwa uwezo wake mkubwa na hasa hasa ’ umahiri ’ wa Kabila lake ( na la GENTAMYCINE ) lililobarikiwa la ’ Tutsi ’ basi Afrika tutawazidi ’ Kimaendeleo ’ Wamarekani, Waingereza, Wachina, Wafaransa, Warusi, Wakorea Kusini na Wajerumani japo najua kwa Waisraeli hatutowaweza kwasababu ambazo hata katika Kitabu Kitukufu na Kilichotukuka cha Biblia zimeelezwa sana tu.
Kama Rwanda sasa tumeanza Kutengeneza Gari aina ya Volkswagen nina amini muda si mrefu tutaanza Kutengeneza Ndege, Mabomu ya Kiwango cha Kimataifa na Hatarishi na ikibidi tutaweza hata Kuwajengea Watu fulani Meli imara ili yasije yakawatokea tena yale ya May 21, 1996 Ziwa Victoria.
Na pengine Rwanda kwa uwezo Wetu mkubwa wa ’ Akili / Upeo ’ unaongozwa na Rais Kagame tunaweza pia hata kufikiria Kuwajengea Wakulima fulani wa nchi fulani ( jirani tu hapa nasi ) Viwanda mbalimbali vya Kubangua na Kupakia ’ Korosho ’ zao ili Watu wao wasiwe wanatupigia sana Kelele wakiwa Dodoma na kutusumbua Sisi ambao muda mwingi tunataka ’ utulivu ’ kwa kuwa tunafikiri sana.
Endeleeni tu ’ Kutuchukia ’ Rwanda na Rais wetu wa Rwanda Paul Kagame ila mkae mkijua kuwa ni Mataifa mawili tu Duniani yana ’ mkono ’ wa baraka za Mungu nayo ni Israeli na Rwanda.
Mtanuna na Mtaninunia sana mwaka huu ila hakuna kama Rwanda na Rais Paul Kagame Afrika.
Ila sijajua itakuwa vipi haya magari,maana nimeisoma BBC leo wanasema kwa mtu wa chini kununua hiyo gari itakuwa kama ni ndoto,maana VW Polo kwa bei ya kiwandani ni $15,000…
[FONT=tahoma]Mkuu Gentamycine pongezi kwa mabandiko yako naomba kuuliza Rwanda wanatengeneza hizo VW au wanaunganisha tu? Kingine kumbe mwenzetu ni wa kutoka kwa PK mwizi wa madini na mfarakanishi wa migogoro inayoendelea Congo-Kinshasa ili afaidike na sahv naambiwa amaeingia Mirerani.[/FONT]
Hivi mkuu zamani JWTZ walitengeneza gari aina ya nyumbu. Hayo magari yaliishia wapi na kwanini hayakuendelea kutengenezwa? Najua ww ni mtu wa Musoma una vinasaba na ujeda, huenda unajua lolote.
Mkuu nakushagaa wewe kumshangaa GENTAMYCINE kuwa ni wa PK. Nakuomba fungua macho na ujiridhishe kuwa Magu ni wa PK. Tuna kazi ya kujikomboa toka kwa haya majitu ya Hima Empire. Sisi eti ni waoga na wajinga hadi tunatawaliwa na mtu mwenye faili Mirembe. Ni dharau kubwa mno. Ila mdogo mdogo tu, maana sisi huku kaskazini tunapambana, naamini Mungu anajua tunachopigania. Atatenda kwa wakati wake.